Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wilaya 27 hazina mahakama za wilaya-Dk. Mahiga
Habari Mchanganyiko

Wilaya 27 hazina mahakama za wilaya-Dk. Mahiga

Spread the love

SERIKALI imesema, ni kweli Wilaya ya Itilima kwa sasa haina Mahakama ya Wilaya, hivyo wananchi wanalazimika kusafiri kwa umbali wa kilometa 37 kufuata huduma katika Wilaya ya Bariadi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Hayo yameelezwa leo tarehe 11 Agosti 2019 bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Gimbi Masaba (Chadema).

Katika swali na msingi la mbunge huyo, alitaka kujua ni lini serikali itajenga mahakama ya wilaya katika Wilaya ya Itilima?

Dk. Mahiga akijibu swali la msingi amesema, ni kweli wilaya hiyo haina Mahakama ya Wilaya na wananchi wanalazimika kusafiri kwa umbali wa kilometa 37 kufuata huduma katika wilaya ya Bariadi.

Aidha, amesema kuwa changamoto hiyo ipo katika wilaya 27 nchini ambazo zinapata huduma katika wilaya za jirani, na hali hiyo inatokana na ukweli kwamba Mahakama ya Tanzania bado inakabiliwa na uhaba wa majengo katika maeneo mengi.

“Kama ambavyo nimekuwa nikieleza katika bunge lako tukufu, mahakama imejiwekea mkakati wa kutatua changamoto hii, hatua kwa hatua kupitia mpango wake na miaka mitano ya kujenga na kukarabati majengo ya mahakama kwa ngazi zote.

“Mahakama ya Wilaya ya Itilima ipo katika mpango wa kujengwa katika mwaka wa fedha 2019/20 pamoja na mahakama nyingine katia wilaya ya Busega, Kyerwa, Misenyi, Gairo, Mbogwe, Songwe,Nyang’wale,Mvomero pamoja na wilaya nyingine zenye uhitaji” ameeleza Dk. Mahiga.

Aidha amesema, anashukuru uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Itilima kwa kutoa kiwanja cha kujenga mahakama ya wilaya, chenye ukubwa za mita za mraba 5,028.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Somo la dini: Waislamu waishukia Serikali, wizara yatoa kauli

Spread the loveJUMUIYA na Taasisi za Kiislamu Tanzania, imetupia lawama Serikali ikidai...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!