BERNALD Nyambari, aliyekuwa Msaidizi wa Upepeli Mkoa wa Kipolisi Kinondoni na shahidi namba nane wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi namba 112/2018, inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake wanane, amehojiwa unadhifu wake? Anaripoti Faki Ssosi…(endelea).
Wakili wa utetezi Peter Kibatala, leo tarehe 11 Agosti 2019 amemhoji Nyambari “kwanini hukuvaa vesti?” ili aonekane nadhifu mahakamani.
Ilikuwa ni awamu ya pili ya maswali baada ya mapumziko kwenye kesi hiyo inayowahusu Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Dk. Vicent Mashinji, Katibu Mkuu-Taifa; John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu – Bara na Salumu Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu -Z’Bar.
Wengine ni Ester Matiko Mbunge wa Tarime Mjini; Halima Mdee, Mbunge wa Kawe; Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini; John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini na Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini.
Mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo;-
Kibatala: Ni sahihi kuwa ofisa wa polisi lazima awe nadhifu?
Shahidi: Polisi lazima awe nadhifu
Kibatala: Mwambie hakimu kwanini hujavaa vesti?
Shahidi: Sifahamu kifungu chochote kinachosema nikivaa nguo za kirai lazima nivae vesti
Kibatala: kwanini hukuvaa vesti?
Shahidi: Ni utashi wangi
Kibatala: Kwanini hujachomekea?
Shahidi: Sipendelee kufanya hivyo
Kibatala: haya…. Nimekusikia sahihi kwamba Akwelina alipigwa risasi?
Shahidi: taarifa nilizonazo alikufa kwa kupigwa risasi
Kibatala: Ni Sahihi kwa taarifa ulizonazo wewe Akwelina alipigwa risasi kwenye tukio linalohusisha washtakiwa
Shahidi: Ni sahihi kwamba alipigwa risasa kwenye tukio hilo
Kibatala: Ni sahihi kwamba bint huyo Mungu amrehemu, alipiga risasi akiwa anaelekea kwenye shughuli zake?
Shahidi: Nilieleza alikuwa kwenye shughuli zake
Kibatala: Ni sahihi kwamba wale waandamanaji walikuwa na mawe, fimbo pamoja na chupa za maji tu?
Shahidi: Vifaa vinavyoneka
Kibatala: vifaa ulivyovitja
Shahidi: ndio vifaa vilivyokuwa vinaonekana
Kibatala: Wakati unaongozw na Wakili wa Serikali uliongozwa kusema waandamanaji walikuwa na bunduki
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Ulifanya zoezi la utambuzi uliwatambua watu wafuatao ni Mbowe, Mashinji, Mdee na Mnyika Spefical kama ulisema lolote juu ya kuwa walikuwa na bunduki?
Shahidi: Sikusema
Kibatala: mwambie hakimu husema chochote juu ya kupatika kwa bunduki au bastola eneo la tukio
Shahidi: Hakuna bunduki au bastola iliyopatika
Kibatala: Katika Upelelezi wako ulisema ulifanya uchunguzi wa kuona, mwambie hakimu kama uliokota maganda ya risasi eneo ambalo ulisema umeokota chupa
Shahidi: Sikusema chochote kuhusiana na maganda ya risasi
Kibatala: Ni Sahihi mawe, chupa za maji ma vifaa vilivyoachwa kwene eneo la tukio
Shahidi: ndio
Kibatala: Mwambie hakimu kama uliongozwa kusema chochote juu ya ukaguzi silaha wanazomiliki kihalali waandamani mmoja au wengi
Shahidi: Sikusema chochote
Kibatala: Shahidi je, kati ya wale uliwataka Mbowe, Mdee, Mashinji na Mnyika uliongozwa kuhusiana na kukagua Silaha zao kwamba kuna mmoja alifyetua?
Shahidi: Sikusema chochote
Kibatala: Unafahamu au hufahamu hao washtakiwa wanamiliki silaha?
Shahidi: Nafahamu Mbowe anamiliki Silaha
Kibatala: aina gani
Shahidi: Belleta
Kibatala: hujaifanyia ukaguz?
Shahidi: Sijaifanyia
Kibatala: Unafahamu kama Mbowe alikuwa na hiyo silaha wakati wa tukio?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Eneo la tukio kulikuwa na Polisi wenye silaha wangapi?
Shahidi: wengi kama watano
Kibatala: aina gani?
Shahidi: SMG
Kibatala: Uliongozwa kusema chochote juu ya hizo silaha tano kuzikagua pengine zilimpiga Akwelina?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Alipigwa risasi eneo gani huyo marehemu?
Shahidi: Alipigwa risasi kichwani
Kibatala: alipigwa kwa umbali au ukaribu?
Shahidi: siwezi kujua
Kibatala: uliongozwa kusema chochote kuhusiana na majerani waliokaa karibu kwenye daladala na Akwelina waliongea chochote kwenye upelelezi wako?
Shahidi: sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kusema chochote juu ya maofisa wa polisi kuhusishwa na kumpiga risasi Akwelina?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Wewe ni mwanasheria maana ya maneno ya kuambiwa unafahamu?
Shahidi: ndio
Kibatala: Nikisema ni umbea nitakuwa sahihi?
Shahidi: sio sahihi ni maneno ya kusikia kwa watu wengine
Kibatala: wewe binafsi uliwasikia washtakiwa kwenye viwanja vya buibui wakitoa maneno ya uchochezi?
Shahidi: sikuwepo
Kibatala: wewe binafsi uliwasikia wakitoa maneno ya kujaza chuki?
Shahidi: sikuwasikia moja moja kwa moja kwa sababu
Hakimu: hiyo sababu iache
Kibatala: Wakati unaongozwa jana na leo Dada yangu alikonesha hati ya mashtaka na kuongozwa maneno hayo wameyasema huyo na huyo
Shahidi: sikuongozwa
Kibatala: Hapo awali uliwataja ni nani na nani alikuwepo kwenye viwanja vya Buibui?
Shahidi: unataka niseme nani na nani au?
Kibatala: Hapo awali uliwataja ni nani na nani alikuwepo kwenye viwanja vya Buibui?
Shahidi: Niliwataja kwa jumla kama sikutaja huyo alikuwa Buibui au Mkwajuni kama unataka niende spesific
Kibatala: Ulisema kwamba moja ya vyanzo vyako ni Bloggs.
Hakimu Simba aliahirisha kesi kuanzia saa 6 na nusu hadi saa saba na kisha Wakili Kibatala aliendelea
Kibatala: Shahidi ni sahihi maneno uliyodai yametamkwa uliyasikia kwenye Bloggs?
Shahidi: Ni pamoja na kwenye Bloggs na kupitoa recods zilizofanywa kwenye mikutano
Kibatala: Mwambie mheshimiwa hakimu iwapo kuna Blogg iliitaja?
Shahidi: Hakuna Blogg niliyoitaja
Kibatala: Shahidi unafahamu kwamba Blogg ili iitwe Blogg kisheria lazima ipitie taratibu fulani za kisheria pale TCRA?
Shahidi: Nafahamu lazima isaijiliwe TCRA
Kibatala: Sasa Shahidi unafahamu Usajili uniafanya Blogg kuwa Safy kwenye mikono ya TCRA?
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Kwa ushahidi wako wewe moja ya ushahidi wako ni Blog tuashumu Blog hiyo imesajili swali langu pamoja na hayo yote uliongozwa kusema kuwa maneno niliyoyasikia ni haya hata kama sio neno kwa neno lakini ni maudhii
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Ndio maana nakueleza hear say ni umbea… katika hizo rekodi uliwahi kuona maandamano yakioneshwa waandamanaji wakiwa kwenye Bararaba ya Kawawa
Kibatala: Mwambie hakimu uliona mwaka gani?
Shahidi: Tarehe 18 Februali kupitia Muungwana Blogg
Kibatala: Uliwahi kuzungumza na mtu wa Muungwana Blogg?
Shahidi: Nilizungumza na Mwandishi anaitwa Charles
Kibatala: Ni ushahidi wako kwamba Charles ndiye aliyepiga picha yeye binafsi na kuziweka Muungwana Blog?
Shahidi: ndoo
Kibatala: Je kuna mtu mwengine aliyepiga picha zaidi ya Charles?
Shahidi: Hakuna mtu mwengine
Kibatala: Uliongea na Charles baada ya kuona Muungwana Blog au kabla?
Shahidi: Niliongea baada ya kuona
Kibatala: Unamjua mkurugenzi wake?
Shahidi: Mkurugenzi Ofisi namjua mtu mmoja anaitw Rashid
Kibatala: Ni muasia au mweusi?
Shahidi: anaonekana kama mwarabu
Kibatala: Twende kwenye Contet (maudhui) ya kile ulichokiona, mwambie hakimu kama ulioneshwa contet zile angalau kuzitambua ili uzitambue
Shahidi: hapana
Kibatala: Shahidi ukitoa uliyoiona Muungwana Blog uliwahi kuona video iliyopigwa na Ofisa wa Polisi anayefanya kazi Ofisi ya RCO?
Shahidi: Sijawahi kuona.
Kibatala: Uliwahi kuongea na Ofisa yoyote wa Polisi kama mpelelezi aliyepiga picha hizo?
Shahidi: Niliongea naye
Kibatala: Anaitwa nani?
Shahidi: Charles
Kibatala: Ulimuhojia tarehe ngapi mwezi gani?
Shahidi: baada ya kutokea tukio hilo
Kibatala: kwa ushahidi wako kama mpelelezi ulimuhoji shahidi bila kuona kile alichokwenda kufanya
Shahidi: Nimhoji yeye kama shahidi na juu ya alichofanya kwenye alichopiga picha
Kibatala: Shahidi Twende pale Kawawa ulipofika ulikuta mabom shapigwa ua yalishapigwa
Shahidi: nilikuwata mabom yanaanza kupigwa
Kibatala: Ni Ushahidi wako wakati linatolewa tangazo la ILANI ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Tusaidie kazi ya ILANI nini kisheria
Shahidi: Ni kuwatawanya watu waliokusanyika kinyume cha sheria
Kibatala: Kuna kosa linafanyika kama ILani imetolewa na watu wamekusanyika
Shahidi: ni sahihi.
Kibatala: Shahidi kubishana na askari kabla ya Ilani ni kosa
Shahidi: sijasema kama watu walibishana na Askari
Kibatala: mheshimiwa naomba jibu lake liingie hivyo hiyo. Wewe ulitokea upande gani wa Moroko wa Magomeni?
Shahidi: Nilitoka eneo la tukio upande mwengine wa barabara
Hakimu: Ulitokea wapi?
Shahidi: ngoja nielezee ukiwa unatoka moroko unakwenda magomeni ukipata kituo cha basi cha Mkwajuni eneo la Hananasof lipo upande wa kushoto kama unatoka Moroko kwenda magomeni?
Kibatala: Kama nakuelewa vizuri kuna barabara ya tatu eneo la mkujuni
Shahidi: Kina Feeder road
Kibatala: ukitokea huko waandamanaji uliwapita au uliwaface
Shahidi: Niliwapita niliacha gari niliingia kwa mguu
Kibatala: Nichoree picha wakati mabomu yanapigwa ulikuwa upo kwenye kundi la Polisi au hujawafikia Polisi
Shahidi: Nilikuwa nawakaribia Polisi
Kibatala: mabomu yalipopigwa watu walitawanyika au hakutawanyika?
Shahidi: baadhi walitawanyika
Kibatala: Ni sahihi ulikuwa na askari wawili wanakusindikiza
Shahidi: sahihi
Kibatala: na Ulisema watu walikuwa wanamawe fimbo na wanaimba kisharishari
Shahidi: sahihi
Kibatala: hawa askari walikuwa wamevaa sare au kirai
Shahidi: kiraia
Kibatala: Hivi ukiwa umevaa kirai unaruhusiwa kumkamata mtu?
Shahidi: Unaruhusiwa kumkamata.
Kibatala: Shahidi wale waandamanaji wale waandamanaji walikuwa wameshika chupa walikuwa wamefanya kosa la jinai au hawakufanya kosa la jinai?
Shahidi: Walifanya kosa la jinai
Kibatala: Naomba umwambie Hakimu iwapo mulimkamata mwandamanaji mmoja au wawili
Shahidi: hatukumkamata mwandamanaji yoyote.
Kibatala: Baada ya mabom kupigwa ulikama waandamanaji au hamkumata
Shahidi: Ulikuwa unamaanisha sisi tuliovaa kiraia au wengine
Kibatala: nimekuuliza spesifical nyie watatu kuna mtu yoyote muliyemkamata
Shahidi: hakuna
Kibatala: Mulimshuhudia askari yoyote anamkamata mtu ambaye amekamatwa na chupa au fimbo
Shahidi: Nimeshuhudia
Kibatala: Swali langu lina sehemu mbili : mwambie hakimu ukitoa hawa watuhumiwa ulisema kulikuwa na waandamanaji 550 je unawafahamu wengine waliokamatwa?
Shahidi: Siwafahamu kwa majina
Kibatala: Hawa waandamanaji unafahamu walikuwa wa kundi gani Yanga, Simba , CCM au CUF?
Shahidi: Siwafahamu
Kibatala: Kabla ya siku ya tukio ulishawahi kupita Hananasif kutoka Mkwajuni
Shahidi: Nishawahi kupita
Kibatala: Ilikuwa shughuli za kipelelezi au Shughuli binafsi
Shahidi: Shughuli binafsi
Kibatala: Uliongozwa na mawakili wa Serikali kutofautisha wingi wa watu na matukio na shughuli
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Shahidi katika hawa watu uliowahoji uliongozwa kusema kuwa ulimuhoji Dereva wa Mwendo kasi?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kufafanunua kama ulimuhoji dereva wa Dalala akawa blocked na waandamanaji
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kufafanunua kuhusu dereva yoyote aliyekuwa akipita hiyo nji
Shahidi: sikuongozwa
Kibatala: Madereva wa Amburance mulisema walikuwa blocked uliongozwa kusema chochote kuhusiana na kumhoji aidha eneo la tukio au kwenda kwenye hospitali ya Mwananyamala sambamba na namba za Amburance?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kusema chochote kuhusu kuwahoji hawa wamiliki wa hizi meza zilizopinduliwa?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kusema chochote juu ya Abiria wa mwendekosa aliyekwama kituo kutokana na athari za maandamano
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Ulisema kuwa baada ya tukio ulifanya zoezi la kuhoji watu ni sahihi
Shahidi: Niliwahoji
Kibatala: Ulianisha hawa watu uliowataja kwa majina kwamba maduka yao yalifungwa katika ushahidi wako ulianisha migahawa na maduka yaliyofungwa
Shahidi: Sikufanya hilo zoezi
Kibatala: hawa washtakiwa wanne walikamatwa kwenye tukio
Shahidi: hawakukamatwa
Kibatala: ulisema kulikuwa na askari wangapi kadiria kama ulivyokadiria wingi wa watu
Shahidi: kama askari 15
Kibatala: hawa Koplo Rahimu na Mwenzake uliwakuta eneo la tukio
Shahidi: sikuwakuta
Kibatala: Nani aliyekuambia hawa kina Koplo Rahimu aliumia ni kwa ufahamu wako au kuna mtu alikuambia
Shahidi: Niliambiwa na Ofisa Operesheni
Kibatala: Tuwazungumzie Koplo Rahimu na mwenzake PC Fikiri uliongozwa kitaja Hospitali ambayo uliwahoji?
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Uliongozwa kusema namna taratibu za kitabibu kwa watu majeruhi walivyokupokea na Ofisa tabibu yupi?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa angalau kutaja tarehe uliyowahoji hawa maofisa wawili?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Rahimu na Fikiri walipokuwa Hospital vitanda vyao vilikuwa umbali gani kuanzia hapo ulipo
Shahidi: kama hapa na hapa (akiwa kizimbani alipokaa kama hatua tano )
Kibatala: kama hatua tano
Shahidi: ndio
Kibatala: walikuwa wodi moja
Shahidi: ndio
Kibatala: Tarehe ngapi uliwahoji
Shahidi: tarehe 17 Februari
Kibatala: na uliwahoji wakiwa wanajitambua ni sahihi
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Uliongozwa kusema chochote kushuhudi majeraha ya kichwani
Shahidi: ee wakili aliniuliza waliumia wapi.
Kibatala: Uliongozwa kusema kuwa ulishuhudia wewe mwenyewe fulani aliumia kichwani uliongozwa au hukuongozwa?
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uliongozwa kumhoji dereva kama yupo wa gari liliwapeleka Rahimu na Fikiri hospitali
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: uliongozwa matibabu waliyopata Rahimu na Fikiri
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Raia wangapi walipigwa Risasi Mkwajuni
Shahidi: Sina kumbukumbu
Kibatala: mmoja au wiwili
Shahidi: sina kumbukumbu
Kibatala: unakumbuku juu ya Raia waliweka Polisi kwa zaidi ya siku tano mahabusu?
Shahidi: Sina kumbukumbu.
Kibatala: kuanzia tarehe 16 Februari ulikuwa unafanya kazi angalau mara mbili kwa Mkuu wa Polisi Mkoa Kinondo
Shahidi: nilisema nafanya kazi kwenye Ofisi za Mkuu wa Upelelezi wilaya
Kibatala: Umbali wa Mahabusi na Ofisi za upelelezi Wilaya
Shahidi: Ofisi na Upepelezi zipo kwenye jengo hilo hilo unapita mahabusu unapanda juu ghorofani ofisini kwangu
Kibatala: Ni sahihi kuwa washtakiwa kuhijiwa na wewe?
Shahidi: Mimi nilikuwa sehemu ya mahojiano hayo
Kibatala: hukuongozwa kusema chochote juu watuhumiwa walikana mashtaka yao hasa kuandamana?
Shahidi: sikuongozwa
Kibatala: Hukuongozwa kusema chochote juu ya washtakiwa wengine kusema hawakuwepo
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ni sahihi washtakiwa watano hukuwatambua
Shahidi: Sikuwatambua kwa sababu sikuwaona kwenye maandamano
Kibatala: Uliongozwa kuzungumzia chochote kuhusu Ofisi ya Mkurugenzi
Shahidi: sikuongozwa
Kibatala: ushahidi wako ulisema kuwa waandamanaji walichochewa kwenda kwa Mkurugenzi?
Shahidi: ndio
Kibatala: uliongozwa kusema chochote juu ya kuwahoji Msimamizi wa uchaguzi au Ofisa wa uchaguzi
Shahidi: Sikuongozwa
Kibatala: Uchaguzi ni tukio la kisheria uliongozwa kutoa nyaraka yoyote uliyoonesha kuwepo kwa uchaguzi
Shahidi: Sikuongozwa.
Kibatala: Ulitoa nyaraka yoyote hapa mahakamani uliyokuwa ikonesha juu ya ufungaji wa kampeni?
Shahidi: sikutoa
Kibatala: tuzungumze kuhusu jeshi la Polisi nani analipenda jeshi la Polisi
Shahidi: Wananchi
Kibatala: kuwa na chuki na jeshi la Polisi ni kosa unatii sheria zote
Shahidi: inategemea kama umehamasishwa.
Kibatala: nataka tuchambue kusema nalichukia Polisi ni kosa mimi nikisema hapa nachukia polisi nikitoka nje nitakamatwa?
Shahidi: hukamatwi
Kibatala: kuchukia serikali ni kosa
Shahidi: ni kosa kutokana na kuhamasishwa
Kibatala: unajua watu waliohudhuria buibui hisia zao
Shahidi: sijui
Kibatala: unafahamu wale watu walihudhuria pale buibui wanaichukia serikali ama laa
Shahidi: sijafanya utafiti
Kibatala: Ni sahihi kwamba zamani unaweza kwenda jeshi la Polisi wakato wowote hakuna makamba makamba lakini siku hizi kuna mageti kuna askari na mabunduki mfano pale Osterbay nafahamu kuwa zamani jeshi la Polisi
Shahidi: ni sahihi kuna mabadiliko
Kibatala: Ni sahihi kuwa mwaka 2016 kuna kituo cha Polisi walishambuliwa askari wakafa wananchi wakashangilia mpaka mkuu wa jeshi la Polisi akatoa onyo kwa wananchi wanaoshangiliwa wakamatwe unakumbuka?
Shahidi: nakumbuka
Kibatala: unakumbuka kuna watu walikamatwa na wakashitakiwa?
Shahidi: nakumbuka
Kibatala: wananchi walishangiliwa kuuwa kwa Polisi kabla ya Buibui yaani tukio la 2016 ili kabla ya buibui
Shahidi: kimya
Kibatala: Tukio la wananchi kushangilia askari kuuawa ilikuwa kabla ya Buibui au baada
Shahidi: inategemea mtu mmoja akiandika mtandaoni sio wananchi wote
Kibatala: Tukio la IGP lilikuwa kabla au baada ya tukio la Buibui.
Baada ya kumaliza kuohjiwa na Wakili Kibatala, sasa ikiwa zamu ya Wakili Mwasipu
Mwasipu: Kuna mtu yoyote alikuja kulalamika kuwa meza yake imepinduliwa na mshtakiwa yoyote aliyekuwa mahakama
Shahidi: Hakuna
Mwasipu: kuna raia yoyote aliyekuja Ofisini kwako kulalamika juu ya kupata hofu kutokana na maandamano
Shahidi: walilalamika hawakuja Ofisini kwangu
Mwasipu: Shahidi kuna raia yoyote alikuja kuwa alifunga duka lake kutokana na hayo maandamano
Shahidi: Walilalamika
Mwasipu: Upelelezi umefanyika wapi
Shahidi: Kanda Maalumu ya Dar es Salaam
Mwasipu: Ni sahihi kwamba wewe ndiye uliyapanga askari aliyekuwa akiandika maelezo ya washtakiwa?
Shahidi: Ni mimi ndio niliyepeleleza
Mwasipu: Kwa mara ya kwanza ripoti yako uliipeleka kwa nani
Shahidi: kwa Mkuu wa Polisi Wilaya kisha .
Mwasipu: Computer ya aina gani
Shahidi: Disktop
Mwasipu: wakati zoezi la kuonesha huo mkanda wewe ulihusikaje
Shahidi: Nilikuwepo
Mwasipu: hizo sauti alizorekodi nani
Shahidi: kutoka kwa mwandishi wa muungwana
Mwasipu: huyo mwandishi wa muungwana alikuwepo?
Shahidi: hakuwepo.
Mwasipu: Uliwahi kusikia sababu washtakiwa kuandamana
Shahidi: nilivyowahoji walisema waliandamana kwenda ofisi ya mkurugenzi wa Kinondoni kwenda kuchukua barua za mawakala wao.
Mwasipu: kwa hiyo sababu ni barua ya utambulisho
Shahidi: ndio
Mwasipu: Kwa ufahamu wako watu wakiwa 20 wanakwenda ofisi ya mkurugenzi huku wanaimba au wanakunya maji wanakuwa wamefanya kosa au sio kosa?
Shahidi: inategemea na mazingira wanaweza kufanya kosa ua sio kosa
Mwasipu: kwa hiyo mazingira ya tarehe 16 uliyaona wewe kuwa yalokuwa kosa
Shahidi: yalikuwa kosa.
Mwasipu: Na sababu ya kwanza kwa kuwa walishika fimbo na maji
Shahidi: sio suala la kushika na mawe, walikuwa wengi wameshika mawe
Mwasipu: nilimuuliza hivyo
Hakimu:Swali lako linapendekeza majibu hayi
Mwasipu: nilimuuliza kwa kuwa walishika mawe walifanya kosa
Shahidi: walishika mawe na namna walivyokuwa ndio linakuwa kosa.
Mwasipu: kuna washtakiwa uliwatambua mahakamani hapa Mdee. Mbowe. Mashinji. Na Mnyika hawa uliiowatambua hapa nani alishika mawe na nani alishika fimbo
Shahidi: sikuwaona.
Mwasipu: shahidi umeleta mawe au fimbo hapa mahakamani kuonesha kwamba katika maandamano kulikuwa na mawe na fimbo
Shahidi: sikuleta kwa sababu
Mwasipu: sijauliza sababu, ni sahihi Pc Fikiri na Koplo Rahimu walidaiwa kupigwa na mawe
Shahidi: Sahihi
Mwasipu: hayo mawe umeyaleta
Shahidi: sikuyaleta
Mwasipu: umetamka hapa chanzo cha maandamano hayo ni hutuba zilizotolewa na washtakiwa ni sahihi?
Shahidi: sahihi.
Mwasipu: Wakati unaongozwa uliongozaa kutamka maneno yaliyopelekea watu kuandamana?
Shahidi: Sikutamka
Mwasipu: Shahidi umetoa maelezo yoyote yaliyotolewa na walalamikaji juu ya kuathirika na maandamano
Shahidi: yapo maofisa wa polisi..
Mwasipu: umeyatoa hujayatoa
Shahidi: sijayatoa
Mwasipu: shahidi ulisema umesikia kilele eneo la kawawa
Shahidi: sahihi
Mwasipu: hizo kelele ulijua nani anapiga
Shahidi: sikujua
Mwasipu: Shahidi kupiga kelele ni koda
Shahidi: sikusema mimi kama ni kosa.
Mwasipu: sikiliza swali langu
Shahidi:sio kosa
Wakili wa uteteza Prof. Safari naye akaendelea kumhoji
Profesa Safari : ulisema Akwelina aliketi kwenye daladala uliliona hilo
Shahidi: ndio
Profesa Safari : umeliona wapi
Shahidi: oysterbay
Profesa Safari : Ulisema gari ilitokea magomeni kuelekea Moroko risasi ilipiga upande gani wa daladala
Shahidi: nyuma
Profesa Safari : huyo mmiliki wa daladala muliandika maelezo yake
Shahidi: mimi sikuwa kwenye timu ya upelelezi .
Profesa Safari : dereva wa Dalala uliandika maelezo yake
Shahidi: kama nilivyosema sikuhusika
Profesa Safari : ni lazima Ofisa wa Polisi akiumia apelekwe Hospitali ya Barabara ya Kilwa ?
Shahidi: inategemea.
Profesa Safari : kuna ushahidi umetolewa OC Fikiri na Koplo Rahimu walilazwa wodi tofauti na wewe umesema wodi moja, ukweli ni upi?
Shahidi: wakati nawahoji walikuwa pamoja
Profesa Safari : ukiichukia serikali unakosa manufaa gani
Shahidi: unaweza kufanya vitendo vya uhalifu
Profesa Safari : hayo manufaa mimi nimeuliza manufaa
Shahidi: sijajua manufaa
Profesa Safari : ukiipenda serikali, unapata manufaa gani kuliko miye profesa niliye na wake wawili na benzi?
Shahidi hakujibu, shauri hilo litaendelea kesho tarehe 12 Septemba 2019.
Leave a comment