Thursday , 2 May 2024
Kimataifa

Ratiba mazishi ya Mugabe

Marehemu Robert Mugabe enzi za uhai wake
Spread the love

MWILI wa Robert Mugabe, aliyekuwa Rais Mstaafu wa Zimbabwe unatarajiwa kuwasili nchini mwake tarehe 11 Septemba 2019, ukitokea Singapore alikofariki dunia wakati anapatiwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ratiba hiyo imetolewa jana tarehe 8 Septemba 2019 na Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara ya Kimataifa.

Taarifa ya wizara hiyo inaeleza, shughuli ya kiserikali ya kuuaga mwili wa Mugabe itafanyika Jumamosi tarehe 14 Septemba 2019 katika Uwanja wa Taifa wa Zimbabwe ulioko Harare nchini humo, wakati mazishi yakitarajiwa kufanyika siku ya Jumapili tarehe 15 Septemba 2019.

Hata hivyo, taarifa hiyo haijaweka wazi eneo ambalo rais huyo mstaafu wa Zimbabwe aliyetawala kwa zaidi ya miaka 37, atazikwa.

Taarifa za Mugabe kufariki dunia zilianza kusambaa tarehe 6 Septemba 2019. Kiongozi huyo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 95. Aliiongoza nchi ya Zimbabwe kuanzia mwaka 1980 hadi mwaka 2017 aliondolewa madarakani na jeshi la nchi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!