MAHAKAMA Kuu ya Dar es Salaam leo tarehe 9 Septemba 2019, imetupilia mbali maombi ya Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, likiwemo ombi namba 3 la kutaka kuzuia kuapishwa kwa aliyekuwa Mbunge Mteule wa jimbo hilo kupitia CCM, Miraji Mtaturu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Jaji Sirilius Matupa wa mahakama hiyo amesema, kama angeruhusu kesi hiyo ifunguliwe, mwishowe jimbo la Singida Mashariki lingekuwa na wabunge wawili yaani Lissu wa Chadema na Miraji wa CCM, hivyo kuvunja Katiba ya nchi.
Hata hivyo, Jaji Matupa amemtaka Lissu kubadilisha aina ya maombi yake na kufungua kesi mpya.
Ufafanuzi zaidi wa uamuzi huo unakujia…
Leave a comment