Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 
Habari za Siasa

Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ametangaza kusitisha kutoa karatasi zinazoonesha orodha ya vikao vya shughuli za Bunge. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Septemba 2019 wakati akitoa tangazo kwa wabunge na kueleza, katarasi hizo hazitatumika tena ndani ya ukumbi wa Bunge na badala yake watakuwa wanatumia njia ya kimtandao.

Na kwamba, wabunge watakuwa wakipewa orodha ya shughuli za Bunge kwa kutumia njia ya mtandao.

“Nataka kuwaambia wabunge kuwa katarasi hizi ambazo tunazitumia kama kuonesha orodha ya shughuli za Bunge, leo ndio siku ya mwisho kungia humu ndani.

“Tunaanza na karatasi hizi na kwa maana nyingine tutakuwa tunawatumia kwa njia ya mtandao, sasa waheshimiwa wabunge naomba mhakikishe mnaweka namba zenu za simu vizuri, barua pepe vizuri na lengo ni kuhakikisha meza za wabunge haikai na makaratasi na badala yake zinakuwa nyeupe kabisa,” amesema Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!