Monday , 29 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 
Habari za Siasa

Spika Ndugai atangaza mfumo mpya kazi za Bunge 

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge ametangaza kusitisha kutoa karatasi zinazoonesha orodha ya vikao vya shughuli za Bunge. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 3 Septemba 2019 wakati akitoa tangazo kwa wabunge na kueleza, katarasi hizo hazitatumika tena ndani ya ukumbi wa Bunge na badala yake watakuwa wanatumia njia ya kimtandao.

Na kwamba, wabunge watakuwa wakipewa orodha ya shughuli za Bunge kwa kutumia njia ya mtandao.

“Nataka kuwaambia wabunge kuwa katarasi hizi ambazo tunazitumia kama kuonesha orodha ya shughuli za Bunge, leo ndio siku ya mwisho kungia humu ndani.

“Tunaanza na karatasi hizi na kwa maana nyingine tutakuwa tunawatumia kwa njia ya mtandao, sasa waheshimiwa wabunge naomba mhakikishe mnaweka namba zenu za simu vizuri, barua pepe vizuri na lengo ni kuhakikisha meza za wabunge haikai na makaratasi na badala yake zinakuwa nyeupe kabisa,” amesema Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!