Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mbunge Chadema ahoji miradi ya maji kutokamilika
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge Chadema ahoji miradi ya maji kutokamilika

Bomba la maji
Spread the love

SERIKALI imetakiwa ieleze, ni lini itahakikisha miradi ya maji ambayo inatakiwa kutekelezwa, inatekelezwa kwa wakati. Anaripoti Dandon Kaijage, Dodoma … (endela).

Pia imetakiwa kwa namna gani miradi hiyo itaenda  sambamba na matumizi bora ya fedha, tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo hutumiwa vibaya.

Conchester Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) leo tarehe 3 Septemba 2019 amehoji serikali wakati akiuliza swali la nyongeza.

Mbunge huyo amesema, kwa kuwa serikali imetenga fedha kwa ajili ya miradi ya maji ambayo ni tatizo ya muda mrefu, je serikali inawehakikishiaje wananchi kuwa ni lini miradi hiyo itakuwa imekamilika?

Awali, katika swali la msingi la Mbunge wa Mikumu, Joseph Haule (Chadema) alitaka kujua kama serikali ipo tayari kutenga kiasi cha fedha kwenye bajeti ili kuokoa maisha ya wananchi zaidi ya 35,000.

Akijibu swali la nyongeza la Rwamlaza, Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Awesso amesema, ni kweli kulikuwa na changamoto kubwa ya kukosekana kwa maji na fedha kutotumika kama inavyotakiwa.

Hata hivyo amesema, tatizo kubwa na changamoto iliyokuwa ikijitokeza, ilikuwa ni mfumo na kwa sasa mfumo umebadilishwa na kwamba, tatizo la maji na matumizi mabaya ya fedha itabaki kuwa historia.

Akijibu Sali la msingi Awesso amesema, Kata za Ruaha, Kidodi na Ruhembe ni miongoni mwa kata 18 zilizopo katika Jimbo la Mikumi na upatikanaji huduma ya maji umefikia asilimia 68.

Aidha amesema, ni kweli chanzo cha maji cha Mto Sigaleti ni miongoni mwa vyanzo vinavyopendekezwa kutumika kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji katika jimbo la Mikumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

error: Content is protected !!