Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Manara aburuzwa kortini, adaiwa Mil 83
MichezoTangulizi

Manara aburuzwa kortini, adaiwa Mil 83

Haji Manara
Spread the love

HAJI Manara, Msemaji wa Klabu ya Simba na wenzake watatu, tarehe 6 Agosti 2019 wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kudaiwa Sh. 83.5 milioni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Msemaji huyo na wenzake (Beatrice Ndungu na Palm General Supply), wamefikisha kwenye Mahakama ya Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam wakidaiwa kupokea bidhaa zenye nembo ya Dela Boss bila kufanya malipo yoyote.

Mlalamikaji ni Abu Masoud Al Jahdhamy LLC ambaye anaiomba mahakama kumwamuru Manara na wenzake kumlipa fedha hizo, fidia pamoja na gharama ambazo anamlipa wakili wake.

Abu Masoud ameeleza, kwamba aliwasambazia bidhaa (pafyumu) walalamikiwa zenye nembo ya Dela Boss ambazo zilitengenezwa Dubai akitarajia malipo.

Katika madai hayo namba 128/2019, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Wanjah Hamza mlalamikaji aliingia mkataba na Manara tarehe 19 Desemba 2018 kwa ajili ya kuchapa bidhaa zenye maneno hayo.

Na kwamba, mkataba huo ulieleza kuwa mlalamikaji atachukua asilimia 70 na Manara asilimia 30. Hata hivyo, mkataba huo umeeleza, faida itakayopatikana itafanywa marejesho kwenye mtaji wa mlalamikaji.

Kesi hiyo imepangwa kuendelea kusikilizwa tena tarehe 29 Agosti 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

error: Content is protected !!