Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Michezo Manara aburuzwa kortini, adaiwa Mil 83
MichezoTangulizi

Manara aburuzwa kortini, adaiwa Mil 83

Haji Manara
Spread the love

HAJI Manara, Msemaji wa Klabu ya Simba na wenzake watatu, tarehe 6 Agosti 2019 wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kudaiwa Sh. 83.5 milioni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Msemaji huyo na wenzake (Beatrice Ndungu na Palm General Supply), wamefikisha kwenye Mahakama ya Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam wakidaiwa kupokea bidhaa zenye nembo ya Dela Boss bila kufanya malipo yoyote.

Mlalamikaji ni Abu Masoud Al Jahdhamy LLC ambaye anaiomba mahakama kumwamuru Manara na wenzake kumlipa fedha hizo, fidia pamoja na gharama ambazo anamlipa wakili wake.

Abu Masoud ameeleza, kwamba aliwasambazia bidhaa (pafyumu) walalamikiwa zenye nembo ya Dela Boss ambazo zilitengenezwa Dubai akitarajia malipo.

Katika madai hayo namba 128/2019, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Wanjah Hamza mlalamikaji aliingia mkataba na Manara tarehe 19 Desemba 2018 kwa ajili ya kuchapa bidhaa zenye maneno hayo.

Na kwamba, mkataba huo ulieleza kuwa mlalamikaji atachukua asilimia 70 na Manara asilimia 30. Hata hivyo, mkataba huo umeeleza, faida itakayopatikana itafanywa marejesho kwenye mtaji wa mlalamikaji.

Kesi hiyo imepangwa kuendelea kusikilizwa tena tarehe 29 Agosti 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

error: Content is protected !!