Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mgogoro: Nyumba, mbuzi vyachomwa moto
Habari Mchanganyiko

Mgogoro: Nyumba, mbuzi vyachomwa moto

Spread the love

NYUMBA ya Tryphone Jeremiah, mkazi wa kijiji Kijiji cha Kishanda B, kilichopo kwenye Kata ya Kibale, Kyerwa mkoani Kagera imechomwa moto. Anaandika Mwandishi Wetu…(endelea).  

Pia wanyama wake wameuawa pamoja na migomba, mikahawa yake kukatwakatwa. Waliofanya tukio hilo ni wanakijiji wenzake kutokana na mgogoro wa ardhi.

Taarifa zaidi kutoka kijijini humo zinaeleza, wanakijiji hao zaidi ya 250 walifanya tukio hilo Jumapili wiki iliyopita.

“Wanalalamika kwamba namiliki ardhi kubwa,” amesema Jeremiah akieleza mgogoro wake na wanakijiji wenzake “wamevamia shamba na kufyeka mazao zaidi ya hekta 10.5, wameua mbuzi wangu na kuwachoma moto.”

Amesema, mgogoro wake na wananchi ulianza mwaka 2007 kwa baba yake ambaye alilalamikiwa kumiliki ardhi hiyo. Wakati wanakijiji hao wakifanya uharibifu huo, wachungaji walikimbia kukwepa kuuawa.

Ahmed Msengi, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera ameeleza, mazao ya kahawa, migomba na miti vimeharibiwa vinaya na wananchi hao.

Medius Atanas, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kishanda B amesema, wanakijiji wamekuwa wakilalamikia Jeremiah kumilikisha ardhi kubwa.

Amesema, wanalalamika kumiliki ardhi ambayo si yake hivyo aliamua kufanya vurugu kwa kuchoma nyumba yake, kuua mifugo jambo ambalo halikubaliki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!