Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Magunia  ya mkaa, yageuka jeneza la Naomi
Habari MchanganyikoTangulizi

Magunia  ya mkaa, yageuka jeneza la Naomi

Marehemu Naomi Marijani
Spread the love

NAOMI Orest Marijani (36), mkazi wa Gezaulole, wilayani Kigamboni, jijini Dar es Salaam, aliyeripotiwa kutoweka nyumbani kwake, tokea tarehe 15 Mei mwaka huu, sasa imethibitika kuwa hayuko tena duniani. Amefariki dunia. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

 Anayetuhumiwa kukatisha maisha ya binti huyo mrembo, ni mume wake, Khamis Said Luwongo (Meshack), kufuatia kinachoitwa, “ugomvi wa kimapenzi.”

Mkuu wa upelelezi wilaya ya Kigamboni, SP Thobias Walelo anaeleza kuwa jeshi la polisi, linamshikilia Meshack kwa tuhuma za mauaji ya mkewe, na kwamba baada ya kutekeleza unyama wake huo, aliuchukua mwili wake na kuuchoma moto ili kuficha ushahidi.”

Anasema, “mara baada ya mauaji hayo, Khamis Said Luongo, aliuchukua mwili wa Naomi na kuuweka kwenye shimo alilochimba kwenye banda la kufugia kuku. Baadaye aliweka mkaa gunia mbili na mafuta ya taa na kisha kuwasha moto uliowaka muda mrefu sana na mwili wote kuteketea kuwa majivu.”

Anaongeza, “kutokana hapo, Meshack aliupakia mwili wa marehemu Naomi kwenye gari lake na kuufikisha kwenye shamba analolimili, lililopo eneo la Vikindu, wilayani Mkuranga, mkoani Pwani. Akachimba shimo na kisha kuufikia. Juu ya eneo hilo, akapanda mgomba.”

Naomi Marijani (Sadra), mfanyabiashara na mwenyeji wa mkoa wa Kilimanjaro, ameacha mtoto mmoja, aitwaye Grecious mwenye umri wa miaka saba.

Mkuu wa Upelelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Camilius Wambura, amethibitisha kutokea tukio hilo, na kwamba  tayari mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi mkoa wa Temeke.

Amesema, “tumeanza kuchunguza huyu mwanamke yuko wapi? Amepoteaje? Nini kimefanyika.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

error: Content is protected !!