Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mwanri: Naomba radhi
Habari za Siasa

RC Mwanri: Naomba radhi

Agrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora
Spread the love

AGREY Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa mwanzoni mwa mwezi Aprili 2019 kwamba, Mungu amshukuru Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya za kuliletea maendeleo taifa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mkoani Tabora, Mwanri amesema, hakuna binadamu anayeweza kuchukua nafasi ya Mungu huku akisistiza kwamba, atakua amechuja sana endapo ataamini hilo.

Mwanri amefafanua kuwa, kauli yake haikuwa na maana mbaya bali ilitafsiriwa tofauti na baadhi ya watu.

Amesema, dhamira yake ilikua ni kutaka kuona kwamba Mwenyezi Mungu anamshukuru Rais Magufuli kutokana na mema anayofanya ya kutetea masilahi ya wangine.

“Ila nilichojifunza ni kwamba, inapopelekwa habari inapokelewa na masikio mengi usifikiri hata kama uko sawa itapokelewa hivyo hivyo, bali itapokelewa tofauti.

“Sina cha zaidi ya kuomba msamaha kwa sababu nimeshafafanua na mimi walioninukuu vibaya natangaza kuwasemehe,” amesema Mwanri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!