Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa RC Mwanri: Naomba radhi
Habari za Siasa

RC Mwanri: Naomba radhi

Agrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora
Spread the love

AGREY Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa mwanzoni mwa mwezi Aprili 2019 kwamba, Mungu amshukuru Rais John Magufuli kutokana na kazi anazofanya za kuliletea maendeleo taifa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mkoani Tabora, Mwanri amesema, hakuna binadamu anayeweza kuchukua nafasi ya Mungu huku akisistiza kwamba, atakua amechuja sana endapo ataamini hilo.

Mwanri amefafanua kuwa, kauli yake haikuwa na maana mbaya bali ilitafsiriwa tofauti na baadhi ya watu.

Amesema, dhamira yake ilikua ni kutaka kuona kwamba Mwenyezi Mungu anamshukuru Rais Magufuli kutokana na mema anayofanya ya kutetea masilahi ya wangine.

“Ila nilichojifunza ni kwamba, inapopelekwa habari inapokelewa na masikio mengi usifikiri hata kama uko sawa itapokelewa hivyo hivyo, bali itapokelewa tofauti.

“Sina cha zaidi ya kuomba msamaha kwa sababu nimeshafafanua na mimi walioninukuu vibaya natangaza kuwasemehe,” amesema Mwanri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!