Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Serikali yathibitisha uwepo wa homa ya dengue Dar, Tanga
Afya

Serikali yathibitisha uwepo wa homa ya dengue Dar, Tanga

Spread the love

SERIKALI imetoa taarifa kwa Umma kuwa bado kuna ugonjwa wa homa wa Dengue hapa nchini licha ya kuwa ugonjwa huo, mpaka sasa hakuna kifo kilichotokana na ugonjwa huo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndungulile alisema kuwa serikali inatoa taarifa ya kuwepo kwa ugonjwa wa homa ya dengue hapa nchini na ugonjwa huo umeibuka tena na kuendelea kuthibitishwa nchini hususani katika majiji ya Dar es Salaam na Tanga kuanzia mwezi Januari 2019.

Alisema kwamba hadi kufikia terehe 2 Aprili 2019 kati ya watu 470 waliopimwa wagomjwa 307 wamethibitishwa kuwa na virusi au walishapata ugonjwa wa homa na kati yao hao 252 kutoka Dar es Saalam na 55 wanatoka Tanga.

“Katika jiji la Dar es Salaam wagonjwa wamethibiitishwa katika hospitali ya Mwananyamala, Ilala, Temeke, Vijibweni, Aga-Khani, Regency, IST na Ebrahim Haji.

“Kutoka katika jiji la Tanga wagonjwa wamethibitishwa katika hospitali za Bombo, Aga-Khan, Burhan Street 4 na Safi Medics,” alieleza Dk. Ndungulile.

Aidha alieleza kuwa ugonjwa huo siyo ugonjwa mpya nchini na katika miaka ya 2010, 2013,2014 na 2018 hasa ukizingatiwa uwepo wa mbu ambaye anaeneza ugonjwa huo.

Alieleza kuwa ugonjwa wa dengue unasababishwa na virusi vinavyoenezwa na mbu aina ya “Aedes” ambao ni weusi wenye madoadoa meupe yenye kung’aa.

Alisema kuwa dalili za ugonjwa huo ni homa ya ghafla, kuumwa na kichwa hususani sehemu za mwili, maumivu ya viungo vya mwili na dalili hizo huanza kujitokeza kati ya siku tatu hadi 14 tangu mtu alipoambukizwa na virusi ya dengue.

Alisema kuwa mgonjwa wa homa ya dengue hutibiwa kutokana na dalili zitakazo ambatana na ugonjwa huo kama vile homa, kupungukiwa damu au maji.

Kutokana na hali hiyo wizara inasisitiza wananchi kuhakikisha wanatunza mazingira kwa kuondoa mazalia ya mbu kama vile kufyeka majani, kuondoa madimbwi  kwa kuyafikia na kuondoa vifuu vya nazi au makopo yanayotuamisha maji.

Hata hivyo hivyo Dk. Ndungulie alitoa rai kwa watanzania wote ili waweze kujenga utamaduni wa kupima afya zao pale wanapojisikia kuwa na dalili tofauti badala ya kusubiri madhara makubwa yajitokeze.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!