Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pigo lingine kwa Maalim Seif, mahakama yamtambua Prof. Lipumba  
Habari za SiasaTangulizi

Pigo lingine kwa Maalim Seif, mahakama yamtambua Prof. Lipumba  

Spread the love

HATIMAYE Mahakama Kuu, Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo tarehe 18 Machi 2019 imetoa uamuzi kwamba, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ni mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi (CUF). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akitoa ufafanuzi wakati wa kusoma uamuzi wa mahakama hiyo kuhusu uenyekiti wa Prof. Lipumba, Jaji Benhajj Masoud wa mahakama hiyo amesema, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa haaishi kusajili tu, inaweza hata kufuta chama.

“Nimeridhika na hiki ambacho kimetolewa ndani ya kiapo cha mjibu maombi namba moja (msajili wa vyama saisa) kwamba, kama hana mamlaka ya kukifuta chama basi hana mamlaka ya kumrejesha Profesa Lipumba kwenye kiti chake,” Jaji Masoud na kuongeza;

“Msajili wa vyama vya siasa haishii kusajili chama tu, ndio maana sheria imempa mamlaka ya kufuta chama hivyo basi anamamlaka hayo,” ameeleza Jaji Benhajj Masoud wakati akitoa uamuzi wa uhalili wa Prof. Lipumba kuwa Mwenyekiti wa CUF.

Awali uamuzi wa kesi hiyo ulitarajiwa kutolewa tarehe 22 Februari 2019, iliahirishwa kwa amelezo kwamba, jaji amepangiwa majukumu mengine nje ya mahakama.

Kwenye kesi hiyo Prof. Lipumba alishitakiwa kuwa si mwenyekiti halali wa CUF kwa kuwa, alijiuzulu kwa hiari yake kupitia tamko lake kwa waandishi wa habari hapo tarehe 5 Agosti 2015.

Kwenye andishi lake hilo Prof. Lipumba alisema, hawezi kushika wadhifa huo kutokana na kukosa ushirikiano wa viongozi wenzake.

Alisema namna chama kinavyokwenda, nafsi yake inamsuta kuendelea kuwa kiongozi wake; ila anakusudia kubakia mwanachama muaminifu na iwapo chama kitaridhia awe tu mshauri wake.

Prof. Lipumba alishikilia uamuzi wake wa kujiuzulu licha ya kunasihiwa na viongozi wenzake wa juu akiwemo Katibu Mkuu Maalim Seif Shariff Hamad.

Hukumu hiyo imekuja ikiwa ni siku nne baada ya Prof. Lipumba kuchaguliwa kwa mara nyingine kuwa mwenyekiti wa chama hicho huku Maalim Seif akiwekwa nje ya chama hicho baada ya kambi ya Lipumba kumchagua Halifa Suleiman Halifa kushika wadhiba huo.

Habari zaidi zitakujia…

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!