Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Tangulizi Rufaa ya Mbowe ulinzi mkali waimarishwa
Tangulizi

Rufaa ya Mbowe ulinzi mkali waimarishwa

Spread the love
ULINZI makali umeimarishwa na Jeshi la Polisi na Magereza kwenye Mahakama ya Rufani wakati mahakama hiyo ikijiandaa kutoa uamuzi wa rufaa ya Freeman Mbowe na Esther Matiko. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).

Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)- Taifa na Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini wamepelekwa mahakamani hapo leo tarehe 18 Februari 2019 kwa ajili ya kusililiza uamuzi ya rufaa yao.

Katika Barabara ya kwenda Kivukoni kuanzia kona ya Mahakama ya Rufaa hadi kona ya Mahakama Kuu, Jeshi la Polisi limeweka polisi wake huku wakitembea huku na kule wakiwa na mitutu jambo mbalo si kawaida.

Mbowe na Mtiko walifutiwa dhama yao tarehe 23 Novemba mwaka jana baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kueleza kuwa, walikwenda kinyume na masharti ya dhamana kwenye kesi ya uchochezi inayowakibili.

Leo Februari 18 Mahakama hiyo itaamua aidha kubatilisha katazo la dhamana ya Mbowe  na Matiko au kuendelea kusota mahabusu ambapo katika kesi ya msingi, washtakiwa ni Mbowe na Matiko.

Wengine ni Mbunge wa Peter Msigwa, Iringa mjini; John Mnyika, Mbunge wa Kibamba na Katibu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji.

Pia wamo Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda; Mbunge wa Kawe, Halima Mdee; Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu ambao wote walikuwepo mahakamani.

Katika kesi ya msingi, washitakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari Mosi na 16, mwaka 2018 maeneo ya Dar es Salaam.

MwanaHALISI Online Ipo Mahakamani kukujuza kitachojirili kwenye uamuzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Walimu 5000 Songwe waililia CWT kuwanyima sare

Spread the loveZaidi ya walimu 5000 ambao ni wanachama wa Chama cha...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

error: Content is protected !!