Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Fatuma Karume: Naachia ngazi TLS
Habari za Siasa

Fatuma Karume: Naachia ngazi TLS

Fatuma Karume, aliyekuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS)
Spread the love

FATUMA Karume, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) hatogombea tena nafasi hiyo baada ya kustaafu Aprili mwaka huu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Karume, mwanasheria huyo mwiba kwa Serikali ya Awamu ya Tano na mtoto wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Makamu Mwenyekiti Mstaafi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zabzibar ameeleza kuwa, nguvu kubwa baada ya kumaliza muhula wake wa mwaka mmoja ulioanzia Aprili mwaka jana, itakuwa ni kwenye biashara zao.

Katika orodha ya wanachama wa chama hicho waliojitosa kugombea nafasi hiyo, jina la Karume halikuwemo na alikuwa hajatoa maelezo yoyote.

Ikiwa leo ni tarehe 18 Februari 2019, zimebaki siku tatu kuhitimisha muda uliowekwa na kamati ya uchaguzi wa kuorodhesha majina ya wataowania nafasi hiyo. Kamati hiyo ilieleza mwisho kuwa tarehe 20 Februari 2019 (Jumatano wiki hii) saa 11 jioni.

“Baada ya kumaliza muda wangu wa mwaka mmoja, sitagombea tena. Naelekeza nguvu kwenye biashara zetu,” amesema Karume alipozungumza na mtandao huu na kuongeza;

“Jamaa zangu wamenishauri vizuri kuwa, niwekeze zaidi muda wangu kwenye biashara zetu.”

Karume ndio rais wa kwanza wa TLS mwanamke tangu kuanzishwa chama hicho mwaka 1954 kupitia Sheria ya Bunge ya mwaka 1954 (The Tanganyika Law Society Ordinance 1954).

Katika uchaguzi wa mwaka jana wa TLS, Karume ndiye mgombea aliyejitokeza dakika za mwisho kugombea nafasi hiyo ambapo alimbwaga Godfrey Wasonga, Godwin Ngwilimi na Godwin Mwapongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Jaji Kiongozi akerwa wananchi kukosa imani na mahakama

Spread the loveWATENDAJI wa Mahakama ya Tanzania, wametakiwa kuweka mikakati itakayosaidia kurejesha...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

error: Content is protected !!