Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lataka waliochota Mil 888 wote asakwe
Habari za Siasa

Bunge lataka waliochota Mil 888 wote asakwe

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

BUNGE limeitaka serikali iwachukulie hatua za kisheria wote waliotajwa katika ubadhilifu wa posho ya resheni (posho ya chakula) ya jumla ya Sh 888.5  milioni kwa watumishi wasio askari. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akiwasilisha bungeni taarifa ya shughuli za Kamati ya Hesabu za Serikali kwa mwaka 2018 Mwenyekiti wa Kamati hiyo leo tarehe 1 Februari 2019, Nagwenja Kaboyoka amesema, kufuatia vigezo na mambo ya msingi katika uchambuzi wa taarifa ya CAG, uimebainisha  kwamba, kulifanyika malipo ya pesa hizo kama posho.

Amesema, malipo hayo yalilipwa kwa watumishi ambao siyo askari kinyume na taratibu za Jeshi la Polisi.

Amesema kuwa, Ofisa Masuhuli alifahamisha kamati kuwa hatua za kinidhamu zimechukuliwa kwa kuwasimamisha kazi watumishi wanne  wanaotuhumia kufanya malipo hayo

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Frank Msaki aliyekuwa Mhasibu Mkuu,Ida Moyo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha mishahara,Damian Bupamba aliyekuwa Mhasibu kitengo cha mishahara na Inspekta Mwita Mirambo.

Alisema Ofisa Masuuli alifafanua kwamba watu wengine watatu wasio watumishi  wa serikali walioshirikiana na watumishi hao  wamekamatwa na kupewa dhamana wakati taratibu za kiupelelezi zikiendelea.

Aliwataja watu hao kuwa ni Ibrahim Mlilima,Nassoro Mlilima na Lodrick Massawe.

Na kwamba, hoja ya kamati  katika hili ni pamoja na kugundulika kwa ubadhirifu mkubwa wa fedha za umma tangu mwaka 2016 hadi 2019  na kwamba, watuhumiwa bado hawajafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazowakabili.

Amesema, uchunguzi wa jambo hilo umechukua muda mrefu kukamilika hivyo kuwepo kwa uwezekano wa fedha za umma kupotea bila hatua stahiki kuchukuliwa kwa wahusika.

Mwenyekiti huyo amesema, Bunge linaazimia kwamba serikali iwachukulie hatua kali na za kisheria wahusika waliohusika katika ubadhilifu huo ndani ya kipindi cha miezi miwili.

“Na kutoa taarifa kwa Bunge kuhusu utekelezaji wa azimio hili,”amesema Kaboyoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

7 wafa Ulanga, mbunge alia kutelekezwa na mawaziri, Tanroad

Spread the loveWatoto saba wamepoteza maisha na zaidi ya kaya 70 kukosa...

error: Content is protected !!