Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge: Wadaiwa matrekta ya SUMA JKT wabanwe
Habari za Siasa

Bunge: Wadaiwa matrekta ya SUMA JKT wabanwe

Matrekta yakiwa katika ofisi za SUMA JKT Mwenge
Spread the love

SERIKALI inatakiwa kuchukua hatua dhidi ya wanasiasa wakiwemo wale waliostaafu ambao wameshindwa kurejesha mikopo ya matrekta waliyopata kutoka Shirika la Uzalishaji Mali linaloendeshwa na Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa bungeni na mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka wakati akiwasilisha taarifa ya kazi za kamati hiyo kwa mwaka wa 2018.

Kaboyoka ambaye ni mbunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema kuna limbikizo kubwa la deni linalotokana na hatua ya kutorejeshwa mikopo ambayo kwa sehemu kubwa walionufaika ni wanasiasa.

Wanufaikaji wengine wa mikopo hiyo iliyofikia thamani ya Sh. Bilioni 40 na ambayo ilianza kutolewa mwaka 2011 mpaka 2016, ni taasisi mbalimbali. Taarifa ya Kaboyoka ilisema deni hilo ni la kufikia Juni 30 mwaka 2017.

Alisema uchambuzi wa kamati umebaini kuwa baadhi ya wadaiwa sugu wa mikopo ni viongozi katika serikali wa sasa na waliostaafu.

“Kama jitihada za dhati hazitafanyika kuna viashiria kuwa madeni hayo hayatalipwa na kuiweka Suma JKT katika hali ngumu kiutendaji… kutorejesha mikopo ni ukiukaji wa mikataba na ni kuisababishia hasara serikali,” alisema.

Ndipo alipotoa kauli kwamba, “… Bunge linaazimia kwamba serikali ifanye uchunguzi wa kina ili kubaini taratibu zilizotumika katika utoaji wa mikopo ya matrekta kwa watu na taasisi mbalimbali na ichukue hatua stahiki kwa wahusika wanaodaiwa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!