Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo hawa kutikisa Kisutu leo
Habari za SiasaTangulizi

Vigogo hawa kutikisa Kisutu leo

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na viongozi wengine wakiwasili mahakamani
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo inatarajia kusikiliza kesi ya vigogo tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Anaripoti  Faki Sosi … (endelea).

Miongoni mwa vigogo hao ni Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa; Dk. Vincent Mashinji, Katibu Mkuu Chadema; Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar; Ester Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini; Halima Mdee, Mbunge wa Kawe, John Heche, Mbunge wa Tarime vijijini na Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini.

Viongozi hao wa Chadema wanakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya mikisanyiko isiyoruhusiwa, kuhamasisha chuki, kushawishi watu kutoridhika na hata kula njama.

Viongozi hoa wanatarajiwa kuendelea na utaratibu wa kimahakama kwa kila mmoja kukabiliana na mashitaka yake.

Kumekuwepo na mahudhurio makubwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam kwenye kesi ya kisiasa inayomuhusisha Mbowe na Matiko.

Mbowe na Matiko walifikishwa mahakamani tarehe 23 Novemba 2018 kwa madai ya makosa kadhaa ikiwemo kufanya mkusanyiko usioruhusiwa na baadaye kukataliwa dhamana.

Kesi zingine zinazotarajiwa kusikilizwa leo ni pamoja na ya wafanyabiashara Seth Harbinder na James Rugemarila pia waliokuwa viongozi wa Timu ya Simba, Evans Aveva na Godfrey na Nyange.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!