Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Kombe la Mapinduzi kuanza Januari Mosi
Michezo

Kombe la Mapinduzi kuanza Januari Mosi

Spread the love

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inatarajia kuanza kuchezwa Januari Mosi, 2019 na kumalizika Januari 13, visiwani Zanzibar ambayo itahusisha timu tisa ambazo zitawekwa kwenye makundi mawili huku kundi A litakuwa na timu nne na kundi B timu tano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kundi A litakuwa na timu za Chipukizi, Mlandege, KMKM na Simba, huku kundi B likihusisha bingwa mtetezi wa michuano hiyo katika mwaka uliopita klabu ya Azam FC, Malindi, Yanga, Jamhuri na KVS.

Azam wanatarajia kushuka dimbani Januari 2 kuvaana na Jamhuri, huku Yanga watatupa karata yao ya kwanza Januari 3 watakapowavaa KVS, kwa upande wa Simba watacheza dhidi ya Chipukizi januari 4.

Taarifa kutoka kwa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo imeeleza kuwa mshindi wa kwanza wa michuano hiyo atazawadia kiasi cha Sh. 15 milioni, medali za dhahabu pamoja na kombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!