Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine amnyima usingizi Museven
Kimataifa

Bobi Wine amnyima usingizi Museven

Bobi Wine
Spread the love

Bobi Wine mwanamuziki wa miondoko ya pop na mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda, anamnyima usingizi rais wan chi hiyo Yower Museven. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Rais Museven yupo kwenye harakati ya kuhakikisha Bobi Wine ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi Ssentamu hapati wasaa wa kukutana na waganda wenye uwanja wa siasa na muziki.

Dhamira ya serikali ya Museven imedhihiri jana baada ya kumkatalia kufanya tamasha lake leo lililopangwa kufanyika jana Disemba 26. Aliyetoa marufuku ya onesho hilo alikuwa Emilian Kayima, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini humo.

Sababu iliyotolewa ni kwamba, Bobi Wine hakufuata utaratibu wa kisheria wa kuandika barua ya kuomba ruhusa ili aweze kufanya tamasha hilo.

Hata hivyo, gazeti la Daily Monitor la nchini Uganda liliandika kuwa, mapema leo jana Bobi Wine aliandika kwenye mtandao wa kijamii kuwa, kikosi cha usalama kimevamia tamasha lake la ‘One Love Beach in Busabala’na kuwakamata wafanyakazi wake.

Mwanzoni mwa mwezi Novemba mwanamziki huyo aliruhusiwa kufanya tamasha lake la kwanza kwa sababu lilikuwa la kiburudani na halikuwa la kisiasa.

Maelfu ya watu waliohudhuria tamasha hilo walivaa nguo nyekundu, rangi inayohusishwa na vuguvugu za Bobi Wine. Na pale alipopanga tamasha la pili, serikali imeamua kuzuia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

error: Content is protected !!