Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Kombe la Mapinduzi kuanza Januari Mosi
Michezo

Kombe la Mapinduzi kuanza Januari Mosi

Spread the love

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inatarajia kuanza kuchezwa Januari Mosi, 2019 na kumalizika Januari 13, visiwani Zanzibar ambayo itahusisha timu tisa ambazo zitawekwa kwenye makundi mawili huku kundi A litakuwa na timu nne na kundi B timu tano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kundi A litakuwa na timu za Chipukizi, Mlandege, KMKM na Simba, huku kundi B likihusisha bingwa mtetezi wa michuano hiyo katika mwaka uliopita klabu ya Azam FC, Malindi, Yanga, Jamhuri na KVS.

Azam wanatarajia kushuka dimbani Januari 2 kuvaana na Jamhuri, huku Yanga watatupa karata yao ya kwanza Januari 3 watakapowavaa KVS, kwa upande wa Simba watacheza dhidi ya Chipukizi januari 4.

Taarifa kutoka kwa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo imeeleza kuwa mshindi wa kwanza wa michuano hiyo atazawadia kiasi cha Sh. 15 milioni, medali za dhahabu pamoja na kombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!