Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Ngono, ngono, ngono UDSM
ElimuTangulizi

Ngono, ngono, ngono UDSM

Spread the love

LEO yaweza kuwa siku ngumu kwa utawala na baadhi ya wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) iwapo Dk. Vicensia Shule ataamua ‘liwalo na liwe.’ Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Dk. Shule ameitwa mbele ya kamati ya maadili ya chuo hicho baada ya kufikisha ujumbe kwa Rais John Magufuli na Watanzania wote kupitia mtandao wa kijamii (twitter) akieleza namna vitendo vya ngono vinavyotawala chuoni hapo.

Dk. Shule amethibitisha kupigiwa simu na chuo hicho akitakiwa leo mchana kufika mbele ya kamati ya maadili kutokana na  ujumbe wake unaotikisha mitandao ya kijamii kwa sasa.

Haikuwa lengo lake kufikisha ujumbe huo kwa njia ya Twitter, alipenda kufikisha ujumbe kwa Rais Magufuli moja kwa moja wakati wa uzinduzi wa maktaba mpya chuoni hapo.

Rais Magufuli alikwenda chuo hicho kufungua maktaba hiyo iliyojengwa katika Kampasi ya Mlimani (Mwalimu. Julius K. Nyerere) na kugharimu kiasi cha Sh. Bil 93.6.

Maktaba hiyo kubwa Afrika Mashariki na Kati imejengwa kwa msaada kutoka Serikali ya China na ndiyo maktaba kubwa kuliko maktaba zote ambazo China imezijenga barani Afrika.

Kwa maelezo ya Dk. Shule, mazingira ya siku hiyo yalimuashiria kusitisha mpango wake wa kupeleka ujumbe kwa muhusika (Rais Magufuli) chuoni hapo. Pia alitaka kutumia bango kuufikisha ujumbe huo.

Dk. Shule aliandika kupitia akaunti yake ya twitter  “Baba @MagufuliJP umeingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kufungua maktaba ya kisasa. Rushwa ya ngono imekithiri mno UDSM. Nilitamani nikupokee kwa bango langu ila ulinzi wako umenifanya ninyamae. Nasubiri kusikia toka kwako maana naamini wateule wako ni waadilifu watakwambia ukweli.”

Jana Alhamis aliandika kwenye twetter: “Kwa manusura wa udhalilishaji huu wa kingono, tunakaribia kufika, tutashinda, tutapata ushindi mkubwa!

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!