Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Matiko waruka kihunzi
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Matiko waruka kihunzi

Mahakama Kuu ya Tanzania
Spread the love

JAJI wa Mahakama Kuu, Sam Rumanyika, ametupilia mbali, mapingamizi ya serikali yaliyolenga kumzuia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, kutoka gerezani. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Washinda pingamizi lao mahakamani, kesi yao kuanza kunguruma mchana huu. Mawakili wa serikali hoi.

Kufuatia uamuzi huo, Jaji Rumanyika amepanga kuanza kusikiliza shauri la msingi leo Ijumaa, kuanzia saa nane mchana.

Mbowe na Matiko, waliwasilisha mahakama kuu maombi ya rufaa, kupinga uamuzi wa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri wa kuamua kuwafutia dhamana.

Hakimu Mashauri alichukua uamuzi wa kuwafutia dhamana Mbowe na Matiko, tarehe 23 Novemba. Alidai washitakiwa wamekiuka masharti ya dhamana na wameidharau mahakama.

Akisoma uamuzi wake huo, mbele ya mamia ya wananchi waliokuwa wakifuatilia shauri hilo,

Jaji Rumanyika, alisema kuwa “pingamizi zilizowekwa na serikali hazina msingi.”

Pingamizi hizo ziliwasilishwa juzi mchana na upande wa mashitaka, ukieleza kuwapo mapungufu kadhaa katika maombi ya washitakiwa ya kutaka kurejeshewa dhamana zao.

Miongoni mwa hoja zilizotolewa na upande wa mashitaka, ni kuwa upande wa utetezi, umekosea kwa kutumia kifungu cha sheria Na. 359 na 361 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), kuwasilisha rufaani yao.

Madai hayo yalipingwa na mawakili wa utetezi, Dk. Rugemeleza Nshalla, Peter Kibatala na Jeremia Mtobyesa.

Mbela ya Jaji Rumanyika, mawakili hao walisema, hoja hiyo iliyowasilishwa na wakili mwandamizi wa serikali, Faraja Nchimbi, mepitwa na wakati kwa mujibu wa sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!