Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ
Habari Mchanganyiko

Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ

Dk. Hassan Abbas, Katibu Mkuu wizara ya Habari
Spread the love

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo, Dk. Hassan Abbas amesema ofisi yake inafuatilia sababu ya watumishi wawili wa Kamati ya Kimataifa ya Kuwalinda Waandishi wa Habari (CPJ), kushikiliwa na kuhojiwa na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa Idara ya Uhamiaji nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dk. Abbas ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali katika ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa “Ofisi yangu inafuatilia kujua kwa nini wanaoitwa waandishi wa habari wa CPJ waliruhusiwa kuingia nchini lakini baadaye wakalazimika kuhojiwa na uhamiaji na kuachiwa.”

Watumishi hao ni Mratibu wa Programu Barani Afrika, Angela Quintal na Mwakilishi wa CPJ Kusini mwa Jangwa la Sahara, Muthoki Mumo wameachwa huru baada ya kushikiliwa na Idara ya Uhamiaji, vile vile, taarifa zinaeleza kuwa, hati zao za kusafiria pia wamerudishiwa.

Watumishi hao walikamatwa usiku wa Jumatano wakiwa kwenye hoteli ya Southern Sun na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa serikali, na kuachwa huru baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

error: Content is protected !!