Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe, Matiko kukamatwa
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe, Matiko kukamatwa

Pingu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru kumatwa kwa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa  Chama  cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Ester Matiko, Mbunge wa Tarime Mjini. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).

Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri  leo tarehe 8 Novemba mwaka 2018  ameamuru kukamatwa kwa viongozi hao kutokana na kushindwa kuhudhuria kwenye kesi inayowakabili hapo bila ruhusa ya mahakama.

Taarifa kutoka ndani ya Chadema zinaeleza kuwa, Mbowe amwekenda nchini Afrika Kusini kwa matibabu. Pia mahakamani hapo mdhamini wa kiongozi huyu ameeleza kuwa, yupo nje ya nchi kwa matibabu.

Mdhamini wa Matiko ameieleza mahakama kuwa, mshtakiwa amepata ziara ya kibunge na yuko nchini Burundi pamoja na kuwasilisha vielelezo ikiwamo tiketi ya ndege.

Kesi inayowakabili Mbowe na viongozi wengine waandamizi ni kufanya maandamano yasiyokuwa ni kufanya maandamano bila kibali.

Viongozi wengine kwenye kesi hiyo ni pamoja na Dk. Vicent Mashinji Katibu Mkuu wa Chama Hicho ,Peter Msigwa Mbunge Iringa Mjini, Halima Mdee, Mbunge wa Kawe John Mnyika (Mbunge Kibamba)).

Wengine ni Salum Mwalimu Naibu Katibu wa Chama hicho Zanzibar , John Heche Mbunge wa Tarime Vijijini. na Easter Bulaya (Mbunge Bunda.

Wakati huo huo Wakili Jamhuri Johnson, anayemtetea Mchungaji Peter Msigwa, katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, ametangaza kujiondoa kumtetea kwa madai ya kutorishishwa na mwenendo wa kesi hiyo unavyoendeshwa.

Wakili Johnson amedai kuwa, mwenendo wa kesi hiyo hauridhishi na kwamba hajawahi kukutana na kesi ya namna hiyo kwa miaka 20 ya uwakili wake.

Watuhumiwa wote wamegoma kujibu chochote wakati walipokuwa wakisomewa maelezo ya awali kwa madai hawawezi kueleza chochote kutokana na kutokuwa na wakili wa kuwatetea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!