Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ
Habari Mchanganyiko

Serikali kufuatiliwa sakata la watumishi wa CPJ

Dk. Hassan Abbas, Katibu Mkuu wizara ya Habari
Spread the love

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo, Dk. Hassan Abbas amesema ofisi yake inafuatilia sababu ya watumishi wawili wa Kamati ya Kimataifa ya Kuwalinda Waandishi wa Habari (CPJ), kushikiliwa na kuhojiwa na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa Idara ya Uhamiaji nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Dk. Abbas ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali katika ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa “Ofisi yangu inafuatilia kujua kwa nini wanaoitwa waandishi wa habari wa CPJ waliruhusiwa kuingia nchini lakini baadaye wakalazimika kuhojiwa na uhamiaji na kuachiwa.”

Watumishi hao ni Mratibu wa Programu Barani Afrika, Angela Quintal na Mwakilishi wa CPJ Kusini mwa Jangwa la Sahara, Muthoki Mumo wameachwa huru baada ya kushikiliwa na Idara ya Uhamiaji, vile vile, taarifa zinaeleza kuwa, hati zao za kusafiria pia wamerudishiwa.

Watumishi hao walikamatwa usiku wa Jumatano wakiwa kwenye hoteli ya Southern Sun na watu wanaodaiwa kuwa maofisa wa serikali, na kuachwa huru baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!