Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto

Spread the love

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi ameshindwa kujibu kipengele B kwenye swali la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuhusiana na idadi ya mashauri yaliyofunguliwa katika mahakama za kimataifa, ambayo serikali imeshinda na kushindwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zitto leo tarehe 9 Novemba 2018 amehoji bungeni kuwa, “Je kuanzia mwaka 2000 hadi 2018 kumekuwa na mashauri mangapi dhidi ya Jamhuri ya Muungano, mangapi yameamuriwa, mangapi bado na mangapi Tanzania ilishinda.”

Lakini Prof. Kabudi hakujibu swali hilo, akisema kwamba ni la mtego na hivyo hatauingia kamwe mtego huo.

Prof. Kabudi ameeleza kuwa, serikali haita tamka chochote kuhusu kesi zilizofunguliwa kwenye mahakama za kimataifa, kwa kuwa ikitoa tamko na kuingia katika taarifa za bunge (Hansard) litahatarisha hoja za serikali katika kesi hizo.

“Masuala yote aliyoyasema, yale yaliyo katika mahakama za kimataifa serikali haitamka chochote. Nataka niwambie katika sheria za kimataifa tamko lolote nitakalolifanya hapa likaingia kwenye hansard litahatarisha hoja za serikali kwenye kesi hizo, na mtego huo uwe wa bahati mbaya au wa kutumwa sitaungia kamwe,” amesema Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!