Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu wakana kumuua mwanafunzi
Elimu

Walimu wakana kumuua mwanafunzi

Spread the love

WALIMU wa Shule ya Msingi Kibeta, Respicius Mtaganzira na Herieth Gerald wanaotuhumiwa kumuua kwa kukusudia aliyekuwa mwanafunzi wa shule hiyo, Sperius Eradius, wamekana mashtaka yao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mwalimu Mtaganzira anadaiwa kumsababishia kifo Sperius aliyekuwa anasoma darasa la tano, kwa kumpiga baada ya mwalimu Gerald ambaye ni mtuhumiwa wa pili katika kesi hiyo, kulalamika kwamba amepoteza mkoba wake wakati mwanafunzi huyo alipompokea mizigo yake alipoingia kazini.

hata hivyo baadaye mkoba wake ulionekana. tukio la mauaji ya mwanafunzi huyo lilisambaa kwa haraka kwenye vyombo vya habari na kuzua mjadala kwa wiki kadhaa mfululizo.

Washtakiwa hao leo tarehe 22 Oktoba 2018 walisomewa mashataka yao na hoja za awali na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Athuman Matuma katika Mahakama Kuu Kanda ya Kagera.

Kesi hiyo imehamishiwa Mahakama Kuu ikitokea Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, baada ya upande wa jamhuri kukamilisha ushahidi ambapo leo ilisikilizwa kwa mara ya kwanza.

Mwalimu Mtaganzira na Gerald wameshtakiwa mahakamani hapo kwa kosa la mauaji ya kukusudia, walilodaiwa kutenda tarehe 27 Agosti mwaka huu kwenye maeneo ya shule ya msingi Kibeta.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!