Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Mkuu astukia ufisadi Dodoma
Habari Mchanganyiko

Waziri Mkuu astukia ufisadi Dodoma

Spread the love

KASSIM Majaliwa, Waziri Mkuu amestukia ufisadi wa Sh. 1.2 bilioni  katika sekta ya kilimo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akiwa kwenye ziara  yake wilayani Chamwino, Dodoma Majaliwa amepokea taarifa ya ubadhirifu wa fedha hizo zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya mradi wa umwagiliaji ambazo matumizi yake hayajulikani

Akizungumza na wananchi wa Tarafa ya Mpwayungu, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mpwayungu amemuagiza Dk. Bilinith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amuagize Ofisa Kilimo wa Mkoa huo Bernad Abraham kwenda kwenye mradi huo kwa ajili ya ukaguzi ili kubaini wezi wa pesa hizo.

Wakati huo huo  Waziri Mkuu alivunja kamati ya kusimamia huduma maji ya kijiji cha Mpwayungu na alimuagiza Mhandisi wa Maji wa wilaya ya Chamwino, Godfrey Mbabaye aunde kamati mpya.

Waziri Mkuu alichukua hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na utendaji wa kamati hiyo ambayo ilishindwa kutekeleza majukumu yake ikiwemo ujenzi wa vituo vya kuchotea maji licha ya kukusanya Sh. 20 milioni kwa mwezi, mradi huo unavituo vinne tu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!