Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu wakana kumuua mwanafunzi
Elimu

Walimu wakana kumuua mwanafunzi

Spread the love

WALIMU wa Shule ya Msingi Kibeta, Respicius Mtaganzira na Herieth Gerald wanaotuhumiwa kumuua kwa kukusudia aliyekuwa mwanafunzi wa shule hiyo, Sperius Eradius, wamekana mashtaka yao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mwalimu Mtaganzira anadaiwa kumsababishia kifo Sperius aliyekuwa anasoma darasa la tano, kwa kumpiga baada ya mwalimu Gerald ambaye ni mtuhumiwa wa pili katika kesi hiyo, kulalamika kwamba amepoteza mkoba wake wakati mwanafunzi huyo alipompokea mizigo yake alipoingia kazini.

hata hivyo baadaye mkoba wake ulionekana. tukio la mauaji ya mwanafunzi huyo lilisambaa kwa haraka kwenye vyombo vya habari na kuzua mjadala kwa wiki kadhaa mfululizo.

Washtakiwa hao leo tarehe 22 Oktoba 2018 walisomewa mashataka yao na hoja za awali na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Athuman Matuma katika Mahakama Kuu Kanda ya Kagera.

Kesi hiyo imehamishiwa Mahakama Kuu ikitokea Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba, baada ya upande wa jamhuri kukamilisha ushahidi ambapo leo ilisikilizwa kwa mara ya kwanza.

Mwalimu Mtaganzira na Gerald wameshtakiwa mahakamani hapo kwa kosa la mauaji ya kukusudia, walilodaiwa kutenda tarehe 27 Agosti mwaka huu kwenye maeneo ya shule ya msingi Kibeta.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!