Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Ngoma aendelea kuitia hasara Azam FC
Michezo

Ngoma aendelea kuitia hasara Azam FC

Spread the love

MSHAMBULIAJI wa Azam FC, Donald Ngoma bado ataendelea kuwa nje ya uwanja baada ya kuendelea kutibu jeraha lake la goti lililomsumbua kwa muda mrefu licha ya kwenda nchini Afrika Kusini kwa matibabu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Msemaji wa klabu hiyo, Jaffari Maganga amesema kuwa kwa sasa hawawezi kumtumia mshambuliaji huyo bila kupata kibari kutoka kwa daktari wa timu hiyo ambaye anafahamu lini Ngoma anatakiwa kurudi uwanjani kutokana na ratiba aliyompangia.

“Mshambuliaji huyo anasaubiri tarehe yake ili aweze kurudi uwanjani lakini mpaka sasa wanafanya mazoezi ya utimamu wa mwili kwa hiyo hivi karibuni watawapokea na kujiunga na wenzao,” amesema Jaffar.

Ngoma ambaye alisajiliwa akitokea Yanga mwishoni mwa msimu wa 2017/18 lakini mpaka sasa ajafanikiwa kucheza mchezo wowote akiwa na timu hiyo licha ya viongozi wake kusema itamchukua wiki tatu tu kupona jeraha lake hilo la goti lakini mpaka sasa bado hali tete.

Katika hatua nyingine klabu ya hiyo inatarajia kucheza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya Arusha United inayoshiriki ligi daraja la kwanza kwa ajili ya kuwapa nafasi wachezaji wao ambao hawakuweza kucheza katika michezo miwili iliyopita ya ligi kutokana na kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!