Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa China kutoa msaada wa Bil 60
Kimataifa

China kutoa msaada wa Bil 60

Rais wa China Xi Jinping
Spread the love

RAIS wa China, Xi Jinping amesema serikali yake itatoa dola za kimarekani 60 bilioni katika mpango wake wa miaka mitatu wa ushirikiano na Afrika katika shughuli za maendeleo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Jinping ametoa ahadi hiyo leo Septemba 03 ,2018 wakati akifungua Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaofanyika jijini Beijing nchini China.

Fedha hizo zinatarajiwa kusaidia bara la Afrika katika shughuli za ujenzi wa miundombinu, ushirikiano katika sekta ya biashara na huduma za afya.

Vile vile, Rais Jinping ameahidi kwamba nchi yake itatoa ushirikiano katika kuimarisha amani ya kudumu Afrika, hatua ambayo ni muhimu kwa ustawi wa nchi za Afrika.

Kadhalika, Rais Jinping amesema China itatoa nafasi za mafunzo ya kilimo bora na mafunzo ya ufundi kwa watalaam kutoka nchi za Afrika ili kuchangia katika maendeleo ya uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!