Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa China kutoa msaada wa Bil 60
Kimataifa

China kutoa msaada wa Bil 60

Rais wa China Xi Jinping
Spread the love

RAIS wa China, Xi Jinping amesema serikali yake itatoa dola za kimarekani 60 bilioni katika mpango wake wa miaka mitatu wa ushirikiano na Afrika katika shughuli za maendeleo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Jinping ametoa ahadi hiyo leo Septemba 03 ,2018 wakati akifungua Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaofanyika jijini Beijing nchini China.

Fedha hizo zinatarajiwa kusaidia bara la Afrika katika shughuli za ujenzi wa miundombinu, ushirikiano katika sekta ya biashara na huduma za afya.

Vile vile, Rais Jinping ameahidi kwamba nchi yake itatoa ushirikiano katika kuimarisha amani ya kudumu Afrika, hatua ambayo ni muhimu kwa ustawi wa nchi za Afrika.

Kadhalika, Rais Jinping amesema China itatoa nafasi za mafunzo ya kilimo bora na mafunzo ya ufundi kwa watalaam kutoka nchi za Afrika ili kuchangia katika maendeleo ya uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!