Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani
Kimataifa

Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani

Spread the love

CHAMA kikuu cha upinzani nchini Zimbabwe ‘Movement for Democratic’ (MDC) kimeenda mahakamani kwa lengo la kukata rufaa, ili kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

MDC imeenda mahakamani ikidai kwamba kulifanyika udanganyifu katika matokeo ya urais yaliyompa ushindi Rais Emmerson Mnangagwa.

Kiongozi wa MDC, Nelson Chamisa amesema timu ya mawakili imefanikiwa kuwasilisha nyaraka za kesi hiyo katika mahakama ya kikatiba.

Chamisa amesema madai yao makuu ni mahakama imtangaze mshindi wa uchaguzi wa rais au iitishe ushaguzi mpya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Chamisa kupoteza ushindi kwa kura chache kwenye uchaguzi wa Julai 30 dhidi ya rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.

Matokeo ya tume ya uchaguzi yalionyesha kuwa Mnangagwa alipata asilimia 50.8 ya kura akifuatwa na Chamisa akiwa na asilimia 44.3. Lakini Chamisa anadai alipata asilimia 56 ya kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!