Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani
Kimataifa

Urais wa Mnangagwa wapingwa mahakamani

Spread the love

CHAMA kikuu cha upinzani nchini Zimbabwe ‘Movement for Democratic’ (MDC) kimeenda mahakamani kwa lengo la kukata rufaa, ili kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

MDC imeenda mahakamani ikidai kwamba kulifanyika udanganyifu katika matokeo ya urais yaliyompa ushindi Rais Emmerson Mnangagwa.

Kiongozi wa MDC, Nelson Chamisa amesema timu ya mawakili imefanikiwa kuwasilisha nyaraka za kesi hiyo katika mahakama ya kikatiba.

Chamisa amesema madai yao makuu ni mahakama imtangaze mshindi wa uchaguzi wa rais au iitishe ushaguzi mpya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Chamisa kupoteza ushindi kwa kura chache kwenye uchaguzi wa Julai 30 dhidi ya rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.

Matokeo ya tume ya uchaguzi yalionyesha kuwa Mnangagwa alipata asilimia 50.8 ya kura akifuatwa na Chamisa akiwa na asilimia 44.3. Lakini Chamisa anadai alipata asilimia 56 ya kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!