Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TRA yapewa ushauri kuokoa makusanyo ya kodi
Habari Mchanganyiko

TRA yapewa ushauri kuokoa makusanyo ya kodi

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeshauriwa kuweka mikakati thabiti itakayowezesha kudhibiti upotevu wa makusanyo ya kodi yatokanayo na sekta madini kuanzia kwa wachimbaji wadogo na kuiingizia Serikali mapato. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, Sauda Mtondoo amesema hayo wakati alipotembelea banda la TRA lililopo kwenye maonesho ya wakulima ya Mwalimu Nyerere 88 Kanda ya Mashariki yaliyopo kwenye eneo la Tungi mkoani hapa.

Mtondoo amesema kuwa bila ya kuweka mikakati ya makusanyo kwa sekta hiyo ya madini wanaweza kujenga nafasi kubwa ya upotevu wa mapato kufuatia kwa sasa kushughulika na wachimbaji wenye leseni pekee na kuwaacha wasio na leseni na hivyo kupoteza mapato ya Serikali.

Akizungumzia hilo, Ofisa Huduma na Elimu kutoka Makao Makuu TRA, Patrick Ezekiel amesema, TRA tayari imeshaandaa mipango ya kutathmini shughuli za wachimbaji wadogo wa madini na kisha kuangalia namna ya mapato wanayostahili kuyatoa na kuweza kuingiza serikalini.

Ezekiel amesema, kwa kushirikiana na Wizara ya Madini watahakikisha wanazitambua Sekta husika na kuzirasimisha kwa kuanzia na vikundi vidogo vidogo ambapo tayari wameshaanza na wamachinga.

Amesema, katika sekta ya madini kuna wachimbaji, wachenjuaji, madalali na wasafirishaji ambao wote kwa pamoja wanahitajika kulipa kodi kwa manufaa ya Umma.

Aidha amesema, mpango mkakati wa jinsi ya kufanya makusanyo ya kodi na kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo mtambuka unaweza kutolewa baada ya miezi 2-3 ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!