Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TRA yapewa ushauri kuokoa makusanyo ya kodi
Habari Mchanganyiko

TRA yapewa ushauri kuokoa makusanyo ya kodi

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeshauriwa kuweka mikakati thabiti itakayowezesha kudhibiti upotevu wa makusanyo ya kodi yatokanayo na sekta madini kuanzia kwa wachimbaji wadogo na kuiingizia Serikali mapato. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Mkuu wa Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, Sauda Mtondoo amesema hayo wakati alipotembelea banda la TRA lililopo kwenye maonesho ya wakulima ya Mwalimu Nyerere 88 Kanda ya Mashariki yaliyopo kwenye eneo la Tungi mkoani hapa.

Mtondoo amesema kuwa bila ya kuweka mikakati ya makusanyo kwa sekta hiyo ya madini wanaweza kujenga nafasi kubwa ya upotevu wa mapato kufuatia kwa sasa kushughulika na wachimbaji wenye leseni pekee na kuwaacha wasio na leseni na hivyo kupoteza mapato ya Serikali.

Akizungumzia hilo, Ofisa Huduma na Elimu kutoka Makao Makuu TRA, Patrick Ezekiel amesema, TRA tayari imeshaandaa mipango ya kutathmini shughuli za wachimbaji wadogo wa madini na kisha kuangalia namna ya mapato wanayostahili kuyatoa na kuweza kuingiza serikalini.

Ezekiel amesema, kwa kushirikiana na Wizara ya Madini watahakikisha wanazitambua Sekta husika na kuzirasimisha kwa kuanzia na vikundi vidogo vidogo ambapo tayari wameshaanza na wamachinga.

Amesema, katika sekta ya madini kuna wachimbaji, wachenjuaji, madalali na wasafirishaji ambao wote kwa pamoja wanahitajika kulipa kodi kwa manufaa ya Umma.

Aidha amesema, mpango mkakati wa jinsi ya kufanya makusanyo ya kodi na kuongeza mapato ya Serikali kupitia sekta hiyo mtambuka unaweza kutolewa baada ya miezi 2-3 ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!