MABINGWA wa Tanzania Bara Simba kupitia mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano wao Haji Manara wametangaza vingilio katika tamasha lao kubwa la kila mwaka ‘Simba Day’ ambalo litafanyika tarehe 8 Agosti, 2018 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Vingilio hivyo katika tamasha hilo vitakuwa Sh. 5,000 kwa mzunguko, Sh. 20,000 kwa VIP A na Sh 15,000 kwa upande wa VIP B.
Manara amesema wameweka vingilio vya bei ya chini kwa lengo la kutoa nafasi kwa mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo waweze kupata fursa ya kuja kwa wingi kuisapoti timu yao.
Simba ambao kwa sasa wameweka kambi nchini Uturuki wanatarajia kucheza na klabu ya Asante Kotoko ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu nchini Ghana.
Leave a comment