Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbaroni kwa kujiteka jijini Mwanza
Habari Mchanganyiko

Mbaroni kwa kujiteka jijini Mwanza

Spread the love

Mfanyabiashara Prosper Peniel (26) mkazi wa Kwimba mkoani Mwanza anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa kosa la kutoa taarifa ya uongo kuwa ametekwa na watu wasiojulikana kwa lengo la kuishinikiza familia yake imtumie kiasi cha Sh. milioni 53. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 02 Agosti, 2018 na  Kamanda wa Polisi Mwanza, DCP Ahmed Msangi, ambapo amesema mtuhumiwa huyo alisambaza taarifa hizo tarehe 18 Agosti mwaka huu.

Kamanda Msangi amesema Peniel aliwataka ndugu zake kumtumia kiasi hicho cha fedha ili aachiwe kitendo ambacho ni kosa la jinai.

“Mtuhumiwa alimtumia ndugu yake ujumbe mfupi kupitia simu yake ya mkononi kuwa ametekwa na watu wasiojulikana wakati akitembea kwa miguu katika barabara ya Kenyatta karibu na jengo la NSSF plaza hapa jijini mwanza. Baada ya ndugu zake kupokea taarifa hizo walitoa taarifa kituo cha polisi,” amesema Kamanda Msangi na kuongeza.

“Askari kwa kushirikiana na ndugu wa mtuhumiwa walianza kufanya ufuatiliaji katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mwanza na maeneo ya mikoa ya jirani ili kuweza kubaini wahusika waliomteka mtuhumiwa na mahala alipopelekwa baada ya kutekwa.

“Ndipo tarehe tajwa hapo juu polisi walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa amelala kwenye nyumba ya  kulala wageni ya majani lodge iliyopo wilayani Kwimba  akiwa na simu ya mkononi aliyokuwa akiitumia kutoa taarifa za uongo kwa ndugu na marafiki kuwa ametekwa.”

Kamanda Msangi amesema Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa, na kwamba pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. Aidha uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!