ALIYEKUWA Mbunge wa Ukonga, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mwita Mwaikabe Waitara, kesho Ijumaa, atapokelewa rasmi jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Waitara ambaye aliondoka Chadema Jumamosi iliyopita na kujiunga na Chama Cha Mapimduzi (CCM), anatarajiwa kupokelewa kwenye chama chake hicho kipya, kupitia mkutano maalum wa jimbo la Ukonga.
Kwa mujibu wa Waitara, katika mkutano huo, viongozi kadhaa wa Kata na matawi kutoka jimbo la Ukonga na jimbo jirani la Segerea, wanatajiwa kuondoka na Chadema na kujiunga na CCM.
“Kesho ndio naanza kazi rasmi ya kubomoa Chadema pale Ukonga,” amesema Waitara na kuongeza, “Nataka kuwaonyesha kuwa mimi nina watu na kwamba uamuzi wangu wa kuondoka Chadema ulikuwa sahihi.”
Leave a comment