Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kuanzia soko huria na madini
Habari za Siasa

Serikali kuanzia soko huria na madini

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kuanzisha soko huria la madini (Tanzania Mineral Exchange) ifikapo mwezi Desemba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki wakati akihutubia kwenye kikao cha menejimenti ya wizara ya madini na taasisi zake ambapo wataalamu kutoka Kampuni ya Tanzania Mecantile Exchange PLC-TMC waliwasilisha mada juu ya elimu ya soko la bidhaa Tanzania.

“Natamani kuona ndani ya kipindi cha miezi sita vinavyoweza kufanyika vinaanza kufanyika. Lakini tutazingatia sheria, taratibu na utaalamu kuhakikisha kwamba suala hili linafanikiwa,” amesema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko alimpongeza Waziri Kairuki kwa kuanzisha wazo hilo ambalo litawezesha kuleta mageuzi katika sekta ya madini, na kuwataka wataalamu wa Wizara ya Madini kulichukulia kwa uzito suala hilo ili utekelezaji wake ufanyike kama ilivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!