Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kuanzia soko huria na madini
Habari za Siasa

Serikali kuanzia soko huria na madini

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kuanzisha soko huria la madini (Tanzania Mineral Exchange) ifikapo mwezi Desemba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki wakati akihutubia kwenye kikao cha menejimenti ya wizara ya madini na taasisi zake ambapo wataalamu kutoka Kampuni ya Tanzania Mecantile Exchange PLC-TMC waliwasilisha mada juu ya elimu ya soko la bidhaa Tanzania.

“Natamani kuona ndani ya kipindi cha miezi sita vinavyoweza kufanyika vinaanza kufanyika. Lakini tutazingatia sheria, taratibu na utaalamu kuhakikisha kwamba suala hili linafanikiwa,” amesema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko alimpongeza Waziri Kairuki kwa kuanzisha wazo hilo ambalo litawezesha kuleta mageuzi katika sekta ya madini, na kuwataka wataalamu wa Wizara ya Madini kulichukulia kwa uzito suala hilo ili utekelezaji wake ufanyike kama ilivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!