Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali kuanzia soko huria na madini
Habari za Siasa

Serikali kuanzia soko huria na madini

Spread the love

SERIKALI ina mpango wa kuanzisha soko huria la madini (Tanzania Mineral Exchange) ifikapo mwezi Desemba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki wakati akihutubia kwenye kikao cha menejimenti ya wizara ya madini na taasisi zake ambapo wataalamu kutoka Kampuni ya Tanzania Mecantile Exchange PLC-TMC waliwasilisha mada juu ya elimu ya soko la bidhaa Tanzania.

“Natamani kuona ndani ya kipindi cha miezi sita vinavyoweza kufanyika vinaanza kufanyika. Lakini tutazingatia sheria, taratibu na utaalamu kuhakikisha kwamba suala hili linafanikiwa,” amesema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko alimpongeza Waziri Kairuki kwa kuanzisha wazo hilo ambalo litawezesha kuleta mageuzi katika sekta ya madini, na kuwataka wataalamu wa Wizara ya Madini kulichukulia kwa uzito suala hilo ili utekelezaji wake ufanyike kama ilivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!