Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Omary Kaaya Katibu mkuu mpya Yanga
Michezo

Omary Kaaya Katibu mkuu mpya Yanga

Omar Kayaa
Spread the love

KIKAO cha dharula kilichofanywa na Kamati ya Utendaji na Bodi ya Wadhamini ya Klabu ya Yanga imemteua na kumtangaza Omar Kayaa kuwa Katibu Mkuu wa muda wa klabu hiyo katika kipindi hiki cha mpito baada ya Boniface Mkwasa kujiuzulu nafasi hiyo siku chache zilizopita. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kaaya ambaye hapo awali alikuwa meneja masoko wa klabu hiyo atashikilia nafasi hiyo kwa muda hasa katika kipindi hichi ambacho Yanga inashiriki katika michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuweka maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza Agosti 23, mwaka huu.

Mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Gor Mahia unatarajiwa kuchezwa siku ya Jumapili Agosti 29, katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam majira ya saa moja usiku, huku Yanga ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mchezo uliopita jijini Nairobi kwa mabao 4-0.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

error: Content is protected !!