KIKAO cha dharula kilichofanywa na Kamati ya Utendaji na Bodi ya Wadhamini ya Klabu ya Yanga imemteua na kumtangaza Omar Kayaa kuwa Katibu Mkuu wa muda wa klabu hiyo katika kipindi hiki cha mpito baada ya Boniface Mkwasa kujiuzulu nafasi hiyo siku chache zilizopita. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Kaaya ambaye hapo awali alikuwa meneja masoko wa klabu hiyo atashikilia nafasi hiyo kwa muda hasa katika kipindi hichi ambacho Yanga inashiriki katika michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuweka maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza Agosti 23, mwaka huu.
Mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Gor Mahia unatarajiwa kuchezwa siku ya Jumapili Agosti 29, katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam majira ya saa moja usiku, huku Yanga ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mchezo uliopita jijini Nairobi kwa mabao 4-0.
Leave a comment