Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Michezo Omary Kaaya Katibu mkuu mpya Yanga
Michezo

Omary Kaaya Katibu mkuu mpya Yanga

Omar Kayaa
Spread the love

KIKAO cha dharula kilichofanywa na Kamati ya Utendaji na Bodi ya Wadhamini ya Klabu ya Yanga imemteua na kumtangaza Omar Kayaa kuwa Katibu Mkuu wa muda wa klabu hiyo katika kipindi hiki cha mpito baada ya Boniface Mkwasa kujiuzulu nafasi hiyo siku chache zilizopita. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kaaya ambaye hapo awali alikuwa meneja masoko wa klabu hiyo atashikilia nafasi hiyo kwa muda hasa katika kipindi hichi ambacho Yanga inashiriki katika michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika na kuweka maandalizi kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara unaotarajiwa kuanza Agosti 23, mwaka huu.

Mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Gor Mahia unatarajiwa kuchezwa siku ya Jumapili Agosti 29, katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam majira ya saa moja usiku, huku Yanga ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mchezo uliopita jijini Nairobi kwa mabao 4-0.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!