Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kwachafuka, watimua madiwani wake
Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwachafuka, watimua madiwani wake

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wilayani Mbeya, kimetangaza kuwavua uanachama madiwani wake watatu kwa madai ya “utovu wa nidhamu na kukiuka taratibu za chama.” Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo mjini Mbeya na katibu wa chama hicho wilayani humo. Madiwani waliovuliwa uanachama, ni Newton Mwatujobe kutoka kata ya Manga; Godfrey Kagili (Sisimba) na Humphrey Ngalawa (Lwambi).

Hata hivyo, kwa mujibu wa katiba ya Chadema, wilaya, mkoa na hata Kanda, hazina mamlaka ya kufukuza au kuchukulia hatua za kinidhamu madiwani. Mamlaka ya nidhamu ya madiwani, ni Kamati Kuu (CC).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, mmoja wa madiwani aliyetangazwa kuvuliwa uwanachama ni yule ambaye ameonekana kwenye mitandao ya kijamii akimsifia naibu spika, Dk. Tulia Akcson.

Dk. Tulia anatajwa na baadhi ya watu mkoani Mbeya kuwa amejipanga kumng’oa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!