Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Gari litakaloziisha mzigo faini Mil 34, jela miaka mitatu
Habari Mchanganyiko

Gari litakaloziisha mzigo faini Mil 34, jela miaka mitatu

Spread the love

SHERIA ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inatarajia kuanza kutumika nchini Januari 2019 huku ukomo wa adhabu kwa makosa ya usafirishaji utakuwa ni dola za Marekani 15,000 (zaidi ya Sh. 34 milioni). Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Hayo yamebainishwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Joseph Nyamhanga wakati wa kufungua kikao kazi cha wadau wa sekta ya ujenzi utakaojadili kuhusu kuanza kutumika kwa sheria hiyo.

Amesema sheria hiyo ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2017 katika usafirishaji wa abiria na mizigo kwa njia ya barabara nchini zitaanza kutumika mwakani ikiwa ni kutekeleza matakwa ya Jumuia ya Afrika Mashariki ambapo Tanzania na Burundi bado hawajaanza kuitumia.

“Katika kipindi hiki cha mpito, kazi zitakazofanyika nikutoa elimu kwa jamii ambapo elimu hii itatolewa katika kanda zote na pia kubadili mifumo kwenye mizani ili kwenda sambamba na sheria hiyo.”

Aliongeza: “Kwa kiasi kikubwa sheria hii inafanana na Sheria tunayotumia sasa nchini Tanzania, tofauti katika baadhi ya maeneo,” amesema.

Nyamhanga amesema kwa sheria hiyo mpya ukomo wa mtaimbo wenye matairi mapana utakuwa tani 8.5 badala ya tani 10 za sasa.

“Pia kutakuwa na mfumo wa kuweka kumbukumbu za makosa ya msafirishaji na anayezidisha uzito ambao hatimaye unaweza kusababisha gari kufungiwa kufanya usafirishaji kwa muda au moja kwa moja.”

Nyamhanga amesema kwa sheria hiyo mpya pia kutakuwa na adhabu kwa makosa ya usafirishaji hadi ukomo wa dola za Marekani 15,000 au kifungo kisichozidi miaka 3 au vyote kwa pamoja.

“Aidha, adhabu hizo zitahusu pia watumishi wa mizani wanakula njama na wasafirishaji ili kukwepa kulipa tozo ya kuzidisha uzito. Sheria ya sasa suala la kifungo au vyote kwa pamoja, lakini sasa limeongezwa,” alisema.

Nyamhanga amesema sheria hiyo pia inahusu gharama za utunzaji gari iliyokuwa na makosa katika maeneo ya mizani baada ya siku tatu kulipa ni dola za Marekani 50 kwa siku badala ya dola za Marekani 20 kwa siku kwenye sheria ya sasa.“

Aidha, gharama ya kuendelea kuegesha gari ndani ya yadi ya mizani baada ya kulipa tozo ya uzalishaji uzito ni dola za Marekani 50 kwa siku,” alisema.

Nyamhanga amesema sheria mpya pia inataka wasafirishaji kuhitaji vibali mahususi vya kusafirisha mizigo isiyo ya kawaida katika makundi mbalimbali.

Akifafanua aina ya vibali, Nyamhanga amesema ni kwa mizigo iliyozidi vipimo kwa mujibu wa Sheria na ile ambao unaweza kugawanyika lakini unahitaji umakini zaidi na vifaa maalum katika ushushaji wake.

Pia vibali vitatakiwa kuombwa kwa mzigo ambao haugawanyika na umezidi kiwango cha uzito unaoruhusiwa kisheria na ile ambayo ni hatarishi kwa afya na usalama katika usafirishaji wake kwa njia ya barabara.

“Pia vitaruhusu mzigo ambao unaweza kuhama kutoka sehemu moja ya gari hadi sehemu nyingine wakati gari likiwa kwenye mwendo au limesimama.

Aliongeza: “ Vibali vya kusafirisha mizigo vitalipwa dola za Marekani 10 badala ya dola za Marekani 20 kwenye Sheria inayotumika sasa. Gharama ya vibali imeshuka, lakini kuna masharti makubwa zaidi ili kuzilinda barabara zetu.”

Nyamhanga alisema Sheria ya mpya na kanuni zake ina mashariti magumu na adhabu kali kwa makosa ya uzidishaji uzito wa magari na makosa mengine ya usafirishaji.

Pia alitumia fursa hiyo kuwaasa wasafirishaji kutii na kuzingatia kikamilifu matakwa ya sheria kwa kutozidisha uzito wa magari ili kuepuka adhabu kali, lakini pia kuzifanya barabara zidumu kwa muda mrefu zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!