Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kwachafuka, watimua madiwani wake
Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwachafuka, watimua madiwani wake

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wilayani Mbeya, kimetangaza kuwavua uanachama madiwani wake watatu kwa madai ya “utovu wa nidhamu na kukiuka taratibu za chama.” Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Uamuzi huo umetangazwa leo mjini Mbeya na katibu wa chama hicho wilayani humo. Madiwani waliovuliwa uanachama, ni Newton Mwatujobe kutoka kata ya Manga; Godfrey Kagili (Sisimba) na Humphrey Ngalawa (Lwambi).

Hata hivyo, kwa mujibu wa katiba ya Chadema, wilaya, mkoa na hata Kanda, hazina mamlaka ya kufukuza au kuchukulia hatua za kinidhamu madiwani. Mamlaka ya nidhamu ya madiwani, ni Kamati Kuu (CC).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya chama hicho, mmoja wa madiwani aliyetangazwa kuvuliwa uwanachama ni yule ambaye ameonekana kwenye mitandao ya kijamii akimsifia naibu spika, Dk. Tulia Akcson.

Dk. Tulia anatajwa na baadhi ya watu mkoani Mbeya kuwa amejipanga kumng’oa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!