Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi

Spread the love

MBUNGE wa Chadema jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amesema, ni lazima chama chake kiibuke kidedea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge jimboni Kinondoni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kigogo leo Jumanne, Kubenea amesema, ushindi kwa Chadema unatokana na makosa ya mshindani wao katika kuteuwa mgombea.

“Ni lazima tutashinda uchaguzi huu. Ni kwa sababu, tuna mgombea mzuri ukilinganisha na CCM na kwamba chama hicho tawala kimedharau wananchi,” ameeleza Kubenea.

Amesema, “kuna wanaopita mitaani na kusema, hata tukishinda hatutangazwa. Nataka kuwaambia, hawatujui. Nataka kuwaambia tutashinda na tutangazwa.”

Uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wake, Maulid Said Mtulia, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF).

Kubenea ndiye meneja kampeni wa mgombea ubunge wa Chadema katika jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!