Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi

Spread the love

MBUNGE wa Chadema jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amesema, ni lazima chama chake kiibuke kidedea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge jimboni Kinondoni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kigogo leo Jumanne, Kubenea amesema, ushindi kwa Chadema unatokana na makosa ya mshindani wao katika kuteuwa mgombea.

“Ni lazima tutashinda uchaguzi huu. Ni kwa sababu, tuna mgombea mzuri ukilinganisha na CCM na kwamba chama hicho tawala kimedharau wananchi,” ameeleza Kubenea.

Amesema, “kuna wanaopita mitaani na kusema, hata tukishinda hatutangazwa. Nataka kuwaambia, hawatujui. Nataka kuwaambia tutashinda na tutangazwa.”

Uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wake, Maulid Said Mtulia, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF).

Kubenea ndiye meneja kampeni wa mgombea ubunge wa Chadema katika jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!