Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea: Tutashinda na tutatangazwa washindi

Spread the love

MBUNGE wa Chadema jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amesema, ni lazima chama chake kiibuke kidedea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge jimboni Kinondoni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Kigogo leo Jumanne, Kubenea amesema, ushindi kwa Chadema unatokana na makosa ya mshindani wao katika kuteuwa mgombea.

“Ni lazima tutashinda uchaguzi huu. Ni kwa sababu, tuna mgombea mzuri ukilinganisha na CCM na kwamba chama hicho tawala kimedharau wananchi,” ameeleza Kubenea.

Amesema, “kuna wanaopita mitaani na kusema, hata tukishinda hatutangazwa. Nataka kuwaambia, hawatujui. Nataka kuwaambia tutashinda na tutangazwa.”

Uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Kinondoni unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wake, Maulid Said Mtulia, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Wananchi (CUF).

Kubenea ndiye meneja kampeni wa mgombea ubunge wa Chadema katika jimbo la Kinondoni, Salum Mwalimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!